Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 5:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 kusudi watu wote wamuheshimu Mwana kama vile wanavyomuheshimu Baba. Asiyemuheshimu Mwana, hamuheshimu Baba aliyemutuma.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 5:23
47 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Jina langu mimi ni Yawe; sitamupa mwingine utukufu wangu, wala sifa zangu sanamu za miungu.


Yawe, Mufalme na Mukombozi wa Israeli, Yawe wa majeshi anasema hivi: Mimi ni wa kwanza na wa mwisho; hakuna mungu mwingine isipokuwa mimi.


Kweli wewe ni Mungu mwenye kufichama, Mungu wa Israeli, Mungu mwokozi.


Mutangaze na kusema habari zenu. Mufanye shauri pamoja! Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa? Ni nani aliyesema mambo haya zamani? Haikukuwa mimi Yawe? Hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi! Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi; hakuna mwingine isipokuwa mimi.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


“Yeye anayemupenda baba yake au mama yake kuliko mimi, hastahili kuwa wangu, na yeyote anayemupenda mwana wake au binti yake kuliko mimi hastahili kuwa wangu vilevile.


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


‘Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao. Lakini mioyo yao ni mbali nami.


Basi muwaendee watu wa mataifa yote kusudi wapate kuwa wanafunzi wangu, mukiwabatiza kwa jina la Baba, la Mwana na la Roho Mutakatifu.


Yesu akaongeza kuwaambia wanafunzi wake: “Yule anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; yule asiyewapokea ninyi, hanipokei mimi, na yule asiyenipokea mimi, hamupokei yule aliyenituma.”


Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Musifazaike; mumwamini Mungu, na muniamini mimi vilevile.


Yeye atanitukuza mimi kwa sababu maneno atakayowaambia yatatokana na yale yanayokuwa ndani yangu.


Na yote ninayokuwa nayo ni yako, na yote unayokuwa nayo ni yangu, nami nimetukuzwa kwa njia yao.


Ninawaandikia ninyi wote wapenzi wa Mungu munaokaa Roma, mulioitwa kuwa watu wake watakatifu. Ninawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.


Isaya naye anasema: “Muzao wa Yese atatokea, atatawala watu wa mataifa, nao watamutumainia.”


Lakini sasa kufuatana na vile mumewekwa huru toka utawala wa zambi na kugeuka watumwa wa Mungu, munapata faida ya kuishi katika utakatifu na kwa mwisho kupewa uzima wa milele.


Lakini ninyi sasa hamutawaliwi na hali yenu zaifu ya kimwili, lakini munatawaliwa na Roho Mutakatifu, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu. Na mutu yeyote asiyekuwa na Roho wa Kristo ndani yake, yeye si mutu wa Kristo.


Tunawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.


Basi, kama mukikula au mukikunywa, au mukifanya neno lolote, mufanye yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.


Kama mutu hamupendi Bwana, alaaniwe! Bwana wetu, kuja!


Hamujui kwamba mwili wenu ni hekalu la Roho Mutakatifu anayekuwa ndani yenu, yule muliyepewa na Mungu? Na ninyi si mali yenu wenyewe.


Tulikuwa tumefikiri kwamba tulihukumiwa kufa. Basi, ilitokea hivi kusudi tusijitegemee sisi wenyewe, lakini tumutegemee Mungu tu anayefufua wafu.


Maana upendo wa Kristo unatuongoza sisi tunaokubali kwamba ni mutu mumoja tu ndiye aliyekufa kwa ajili ya watu wote; maana yake wote wanashiriki katika kifo chake.


Ndiyo kusema, Mungu ndiye aliyekuwa akipatanisha watu wote na yeye mwenyewe kwa njia ya Kristo bila kuhesabu makosa yao. Yeye ametupatia ujumbe wa upatanisho.


Ninawatakia neema wale wote wanaomupenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usiokuwa na mwisho.


na kwa sababu hiyo ninapata mateso haya. Lakini sisikii haya kwa ajili ya ile. Maana ninajua ni nani yule niliyemwamini, nami ninahakikisha kwamba anaweza kuchunga kile alichonipa kwa kunilinda mpaka Siku ile ya kurudi kwake.


Na tena wakati Mungu alipomutuma muzaliwa wake wa kwanza katika dunia, alisema: “Wamalaika wote wa Mungu wanapaswa kumwabudu.”


Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.


Lakini muzidi kukomaa katika neema na katika kumujua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Asifiwe, sasa na hata milele! Amina.


Yule anayemukana Mwana, anamukana Baba vilevile, lakini yule anayemukubali Mwana, anamukubali Baba vilevile.


Kila mutu atakayeenda mbali na asiyedumu katika mafundisho ya Kristo, mutu yule hashirikiani na Mungu. Lakini yule anayedumu katika mafundisho yale, anashirikiana na Baba na Mwana vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ