Mukumbuke maneno niliyowaambia kwamba mutumishi si mukubwa kuliko bwana wake. Kama walinitesa mimi, watawatesa ninyi vilevile. Na kama walishika maneno yangu, watashika maneno yenu vilevile.
Kwa ajili ya neno hili Wayuda walitaka tena zaidi kumwua; si kwa sababu ya kuvunja Sheria ya siku ya Sabato tu, lakini vilevile kwa sababu alisema kwamba Mungu ni Baba yake, akijifanya hivi kuwa sawasawa na Mungu.