Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 5:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Yule mutu akaenda kuwaambia Wayuda kwamba Yesu ndiye aliyemuponyesha.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 5:15
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini mutu yule alipoenda, akaanza kutangaza habari zile fasi zote. Na kwa sababu hii Yesu hakuweza kuingia tena waziwazi katika muji wowote, lakini alibaki mbali nayo pahali penye ukiwa. Na watu walimufikia kule kutoka pande zote.


Huu ndio ushuhuda wa Yoane kwa makuhani na Walawi waliotumwa na Wayuda kutoka Yerusalema kumwuliza kwamba yeye ni nani.


“Mukuje mumwone mutu aliyeniambia maneno yote niliyotenda. Huyu si Kristo?”


kwa hiyo Wayuda wakamwambia mutu yule aliyeponyeshwa: “Leo ni siku ya Sabato, na Sheria haikuruhusu kubeba kipoyi chako.”


Basi wakamwuliza kwamba ni nani aliyemwambia kwamba atwae kipoyi wake na aende.


Kwa sababu ile Wayuda wakaanza kumufuatilia Yesu kwa kuwa alifanya mambo haya kwa siku ya Sabato.


Kwa ajili ya neno hili Wayuda walitaka tena zaidi kumwua; si kwa sababu ya kuvunja Sheria ya siku ya Sabato tu, lakini vilevile kwa sababu alisema kwamba Mungu ni Baba yake, akijifanya hivi kuwa sawasawa na Mungu.


Kwa hiyo Wafarisayo nao wakamwuliza namna gani alivyopata kuona. Naye akawaambia: “Alinipakaa matope kidogo kwa macho, nami nikanawa uso na sasa ninaona.”


Yeye akajibu: “Kama yeye ni mwenye zambi, mimi sijui. Neno moja ninalojua ni kwamba mimi nilikuwa kipofu na sasa ninaona.”


Naye akawajibu: “Kweli neno hili ni la kushangaza kusema kwamba hamujui pahali alipotoka, ijapokuwa ameniponyesha macho.


Wakamujibu: “Wewe, uko mwenye zambi kabisa tangu kuzaliwa kwako! Unataka kutufundisha?” Halafu wakamufukuza inje.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ