Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 5:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kisha Yesu akamukuta mutu yule ndani ya hekalu, akamwambia: “Angalia, sasa umepona. Basi usifanye zambi tena, kusudi jambo baya zaidi lisikufikie.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 5:14
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati alipokuwa katika taabu zaidi, mufalme huyu Ahazi alizidi kumwasi Yawe.


Lakini amani ilipopatikana wakatenda zambi tena mbele yako, nawe ukawaacha watiwe katika mikono ya waadui zao wawatawale. Hata hivyo, walipotubu na kukulilia ukawasikiliza kutoka mbinguni. Na kwa kulingana na rehema zako nyingi, ukawaokoa mara nyingi.


Yawe ameniazibu sana, lakini hakuniachilia nikufe.


Maana nimefuata njia za Yawe, wala sikujitenga na Mungu wangu kwa ajili ya uovu.


Nami nitawaangalia kwa majivuno waadui zangu wanaonizunguka. Nitamutolea Yawe sadaka kwa shangwe, ndani ya hekalu lake, nitaimba na kumushangilia.


Mungu analipiza kisasi cha damu iliyomwangwa; wala hasahau hata kidogo kilio cha wenye kuonewa.


Yawe ataniokoa. Nasi tutamusifu kwa nyimbo za vinubi siku zote za maisha yetu, katika nyumba ya Yawe.


Hezekia akauliza: Ni kitambulisho gani kitakachonijulisha kwamba mimi nitakwenda kwa nyumba ya Yawe?


Kuhani atamwangalia yule mutu. Kuhani akiona pamekuwa shimo na nywele za pahali pale zimegeuka kuwa nyeupe, basi, kuhani atamutangaza mutu yule kuwa muchafu. Huo ni ugonjwa wa ukoma ambao umetokana na jipu.


Na kama hata kisha hayo yote bado hamutanisikiliza mukiendelea kunipinga,


Ikiwa mutu anatoa sadaka hiyo kwa kumushukuru Mungu, basi, ataitoa pamoja na maandazi yasiyotiwa chachu yaliyopakwa mafuta, mikate myembamba iliyopakwa mafuta na maandazi ya unga laini uliochanganywa na mafuta.


Halafu anakwenda kutwaa pepo wengine saba wanaokuwa wabaya kumupita, nao wote wanakuja kuingia na kukaa mule. Na hali ya mwisho ya mutu yule inageuka mbaya kuliko hali yake ya kwanza. Na hivi ndivyo itakavyokuwa kwa watu wa kizazi hiki kibaya.”


Yesu alipoona namna walivyomwaminia, akamwambia yule mwenye kupooza: “Mutoto wangu, zambi zako zimesamehewa.”


Lakini mutu yule aliyeponyeshwa hakujua ni nani, kwa maana Yesu alikuwa amekwisha kuondoka katikati ya kundi kubwa la watu waliokuwa pale.


Pale kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa mugonjwa tangia miaka makumi tatu na minane.


Mwanamuke yule akamujibu: “Bwana, hakuna mutu.” Basi Yesu akamwambia: “Mimi vilevile sikuhukumu. Ujiendee, lakini usifanye zambi tena.”]


Kufuatana na hiyo, zamani mulipitisha siku nyingi mukifanya matendo yanayolingana na ya wapagani. Mulizoea kuishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, za ulevi na kuabudu sanamu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ