25 Mwanamuke yule akamwambia: “Ninajua kwamba Masiya anayeitwa Kristo, atakuja. Na wakati atakapokuja atatuelezea maneno yote.”
Nao watu walipokuwa wamekusanyika pamoja, Pilato akawauliza: “Munataka niwafungulie nani kati ya Baraba na Yesu anayeitwa Kristo?”
Pilato akawauliza tena: “Basi munataka nifanye nini na huyu Yesu anayeitwa Kristo?” Nao wote wakajibu: “Atundikwe juu ya musalaba!”
Leo hii Mwokozi amezaliwa kwa ajili yenu katika muji wa Daudi, yeye ndiye Kristo na Bwana.
Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.”
“Mukuje mumwone mutu aliyeniambia maneno yote niliyotenda. Huyu si Kristo?”
Wasamaria wengi wa muji ule walimwamini Yesu kwa sababu ya maneno ya yule mwanamuke aliposhuhudia hivi: “Aliniambia mambo yote niliyotenda.”
nao wakamwambia yule mwanamuke: “Sasa tunaamini, si kwa sababu ya maneno uliyotuambia tu, lakini kwa sababu tumesikia sisi wenyewe na tunajua hakika kwamba huyu ni Mwokozi wa dunia.”