Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 4:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Babu zetu walimwabudu Mungu juu ya mulima huu, lakini ninyi Wayuda munasema kama Yerusalema ni pahali pa kumwabudia Mungu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 4:20
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe alimwambia: “Nimesikiliza wakati uliponiomba na kunisihi. Nimeitakasa nyumba hii ambayo umenijengea kusudi watu waabudu jina langu hapa milele. Nitaichunga na kuipenda wakati wote.


Kisha Daudi akamujengea Yawe mazabahu pahali pale na kumutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani. Akamwomba Yawe, naye akakubali maombi yake kwa kuleta moto kutoka mbinguni na kuteketeza sadaka kwenye mazabahu.


Basi Daudi akasema: “Hapa ndipo pahali ambapo nyumba ya Yawe itakuwa, na hii ndiyo mazabahu ambapo watu wa Israeli watatolea sadaka ya kuteketezwa kwa moto.”


Lakini kisha nilichagua muji wa Yerusalema ukuwe muji ambamo nitaabudiwa, na nilimuchagua Daudi awatawale watu wangu Waisraeli.’


Kisha Yawe akamutokea usiku, akamwambia: “Nimesikia maombi yako na nimechagua pahali hapa pakuwe nyumba yangu ya kunitolea sadaka.


kwa maana nimetakasa nyumba hii kusudi watu waliabudu jina langu hapa milele. Nitailinda na kuipenda siku zote.


Yawe ameuchagua Sayuni, ametaka ukuwe makao yake.


Lakini alichagua kabila la Yuda, mulima Sayuni anaoupenda.


Yawe anasema hivi: Mbingu ni kiti changu cha kifalme, dunia ni kiti cha kupumzikishia miguu yangu. Mutanijengea nyumba ya namna gani basi, pahali nitakapoweza kupumzikia?


Lakini wale wakaaji wakakataa kumupokea Yesu kwao kwa sababu alikuwa katika safari kwenda Yerusalema.


Babu yetu Yakobo ndiye aliyetupa sisi kisima hiki, hata yeye mwenyewe pamoja na wana wake na nyama wake walikunywa maji yake. Wewe unajiona kuwa mukubwa kuliko Yakobo?”


Yawe atakapowafikisha kwenye inchi munayokwenda kurizi, mutatangaza baraka kutoka kwenye mulima Gerizimu, na laana kutoka kwenye mulima Ebali.


“Mukisha kuvuka Yordani, makabila haya yatasimama juu na mulima Gerizimu kwa kubariki watu: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu na Benjamina.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ