Lakini Elisha akamwambia: “Unafikiri roho yangu haikukuwa pamoja nawe wakati mutu yule alipotoka ndani ya gari lake na kuja kukutana nawe? Huu ndio wakati wa kupokea feza na nguo, mashamba ya mizeituni na mizabibu, kondoo na ngombe au watumishi na wajakazi?
Mumoja wao akajibu: “Hakuna anayekuwa upande wake, ee mufalme. Anayefanya vile ni Elisha, nabii anayekuwa kule Israeli. Yeye anamwambia mufalme wa Israeli mambo yote unayosema hata ukiwa katika chumba chako cha kulala.”
Naye akawauliza: “Ni mambo gani?” Nao wakamujibu: “Haujui mambo yaliyomupata Yesu wa Nazareti? Yeye alishuhudiwa na Mungu na watu wote kwamba alikuwa nabii mwenye uwezo katika mambo aliyofanya na kusema.
Yule Mufarisayo aliyemwalika Yesu alipoona vile, akajisemesha: “Kama mutu huyu angekuwa kweli nabii, angetambua mwanamuke huyu anayemugusa ni wa namna gani. Angetambua kwamba yeye ni mwenye mwenendo mubaya.”