Basi kama akiolewa na mutu mwingine wakati mume wake angali muzima, atahesabiwa kuwa muzinzi. Lakini kama mume wake akikufa, yeye anakuwa huru toka Sheria ile iliyomufunga na hata akiolewa na mutu mwingine hatahesabiwa kuwa muzinzi.
Zaidi ya hayo, nimemupata Ruta wa Moabu mujane wa Malona, kusudi akuwe muke wangu. Mapatano haya yatafanya mali ya jamaa ya marehemu na ukoo wake kubakia kwa watu wake katika muji huu. Ninyi ni washuhuda.”