lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”
Lakini Petro akajibu: “Hapana, hata kidogo Ee Bwana! Mimi sijakula bado kitu chochote kisichoruhusiwa kukuliwa, wala chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu.”
Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.
Akasema tena: “Sasa ni mwisho! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Yule anayesikia kiu, nitamupa maji ya kunywa yanayotoka katika chemichemi ya maji ya uzima pasipo kulipa.
Kisha yule malaika akanionyesha muto wa maji ya uzima wenye kungaa kama kioo, uliokuwa ukitiririka toka kwenye kiti cha kifalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo.
Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.
Kwa maana Mwana-Kondoo anayekuwa katikati ya kiti cha kifalme, atawachunga na kuwaongoza kwenye chemichemi ya maji ya uzima. Naye Mungu atawapanguza machozi yao yote.”