Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 3:36 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

36 Anayemwamini Mwana yuko na uzima wa milele. Anayekataa kumwamini Mwana hatapata uzima; atakaa akipatwa na kasirani ya Mungu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 3:36
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu aliniokoa nisiangamie katika shimo; nimebaki muzima na ninaona mwangaza.”


Unawashibisha kwa utajiri wa nyumba yako; unawakunywesha katika muto wa wema wako.


Hata akijitukuza katika maisha haya, na kusifiwa kwa sababu ya kufanikiwa,


Andika: Uwaangalie wenye kiburi, hao wataangamia; lakini wenye haki wataishi kwa kumwamini Mungu.


Hakika hakuna mutu yeyote kati ya watu waliotoka Misri mwenye umri wa miaka makumi mbili na zaidi atakayeona inchi niliyoapa kuwapa Abrahamu, Isaka na Yakobo, kwa sababu hawakunitii kwa ukamilifu.


Halafu hawa watakwenda kwenye nafasi watakapoazibiwa kwa milele, lakini wenye haki wataingia kwenye uzima wa milele.”


Anayeamini na kubatizwa ataokolewa, lakini asiyeamini atahukumiwa.


Nimejionea mwenyewe wokovu unaotoka kwako,


Kila mutu ataona jinsi Mungu atakavyotuokoa.’ ”


Lakini wamoja waliomupokea, ndio wale waliomwamini, aliwapa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu.


Mimi ninawapa uzima wa milele, nao hawatapotea hata milele, wala hakuna mutu anayeweza kuwanyanganya toka katika mukono wangu.


Yesu akamujibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili.”


Muvunaji anakwisha kupokea mushahara, naye anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele, kusudi mupandaji na muvunaji wafurahi pamoja.


“Kweli, kweli ninawaambia: anayesikia neno langu na kumwamini yule aliyenituma, anapata uzima wa milele. Yeye hatahukumiwa, lakini ameponyoka lufu na kupata uzima.


Huu ndio mukate ulioshuka toka mbinguni, nao si kama mukate ule babu zenu waliokula katika jangwa na kufa. Anayekula mukate huu ataishi milele.”


Kweli, kweli ninawaambia: kama mutu akishika maneno yangu, hatakufa hata milele.”


Lakini Wayuda waliokataa kuamini walishawishi watu wa mataifa mengine na kuwasukuma kuwachukia wandugu waamini.


Kwa sababu Sheria inaamusha kasirani ya Mungu. Lakini Sheria haingekuwa, kuvunja Sheria hakungekuwa vilevile.


Sasa kwa kuwa tumehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya damu ya Yesu, inaonyesha zaidi sana kwamba atatuokoa kusudi kasirani ya Mungu isituangukie.


Basi sasa hakuna azabu kwa wale wanaoungana na Yesu Kristo.


Lakini wale wanaotegemea kutimiza yale yanayoamuriwa na Sheria, wamelaaniwa. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Alaaniwe mutu yeyote asiyedumu katika yote yanayoandikwa katika hiki kitabu cha Sheria na kuyatii.”


Mutu asiwadanganye na maneno yasiyokuwa na maana; kwa sababu ya makosa kama hayo, Mungu anawaazibu kwa kasirani yake wale wasiomutii.


na kungojea Mwana wake Yesu kutoka mbinguni. Ni yule Mungu aliyemufufua, naye ndiye anayetuokoa toka kasirani ya hukumu ya Mungu inayokuja.


Kwa maana Mungu hakututayarishia kuangamizwa kwa ukali wa kasirani yake, lakini kuokolewa kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Basi, namna gani sisi tutaponyoka azabu kama hatushuguliki na wokovu mukubwa kama huu? Ni Bwana mwenyewe aliyetangaza kwanza habari za wokovu huu, na wale waliomusikia walihakikisha kwetu kwamba ni za kweli.


Tena ni watu gani Mungu aliowaapia kwamba hawataingia kwenye mapumziko aliyowatayarishia? Si wale waliokataa kumutii?


Basi tunaona kwamba hawakuweza kuingia kwenye mapumziko yale kwa sababu ya kutokuamini kwao.


Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ