Mbele ya kukutengeneza katika tumbo la mama yako, mimi nilikujua; mbele haujatoka katika tumbo, nilikuweka kwa kazi yangu; mimi nilikuchagua kuwa nabii kwa mataifa.
Hili lilikuwa onyo kwa Waisraeli kwamba mutu yeyote ambaye si kuhani, maana yake asiyekuwa wa ukoo wa Haruni asiende kwenye mazabahu kwa kumufukizia Yawe ubani. Kama sivyo ataangamizwa kama Kora na wafuasi wake. Haya yote yalitendeka kama vile Yawe alivyomwambia Eleazari kwa njia ya Musa.
Yoane alipata mamlaka ya kubatiza kutoka kwa nani? Kwa Mungu au kwa watu?” Nao wakaanza kupiga mafikiri pamoja na kusema: “Kama tukijibu kwamba mamlaka yake yalitoka kwa Mungu, atatuuliza: ‘Kwa sababu gani basi hamukumwamini?’
Itakuwa kama vile mutu anayefunga safari. Alipotoka kwake akawaachia watumishi madaraka yake, akimupa kila mutu kazi yake. Vilevile akamwagiza mulinzi wa mulango akeshe.
Kwa njia yake Mungu amenipa neema ya kuwa mutume kusudi niongoze mataifa yote yapate kumwamini na kumutii. Na kwa tendo hilo jina lake lipate kusifiwa.
Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa sawa hivi ninavyokuwa, na neema yake niliyopewa haikukuwa ya bure, lakini nilitumika zaidi sana kuliko mitume wote wengine. Hakika si mimi, lakini ni neema ya Mungu inayokuwa pamoja nami.
Basi, Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi wa Mungu, waliowaonyesha ninyi njia ya kuamini. Tumefanya vile kila mumoja wetu kwa kadiri ya zawadi aliyopewa na Bwana.
Ni nani aliyekuweka kuwa mukubwa kuliko wengine? Si Mungu ndiye aliyekupa vitu vyote unavyokuwa navyo? Ikiwa ni hivi, kwa sababu gani unajivuna kama vile haukuvipewa kama zawadi?
Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa wandugu wote wanaokuwa pamoja nami. Ni mimi niliyeitwa kuwa mutume, si kwa kuchaguliwa na watu, wala kwa njia ya mutu, lakini kwa njia ya Yesu Kristo na ya Mungu Baba aliyemufufua. Tunawaandikia ninyi makanisa ya Galatia.
Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo. Mimi niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi watu wa Mungu munaokaa Efeso, munaokuwa waaminifu katika kuungana na Yesu Kristo.
Ni kwa hiyo nimewekwa kuwa mujumbe na mutume kwa kuwafundisha watu wa mataifa mengine kusudi wapate kumwamini Mungu na kutambua ukweli. Mimi ninasema ukweli wala si uongo.
Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.