Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 3:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Yesu akamujibu: “Wewe unayekuwa mwalimu mukubwa katika inchi ya Israeli, haujui maneno haya?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 3:10
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Umujalie Solomono mwana wangu kusudi kwa moyo wote ashike amri zako, ushuhuda na maagizo yako, atimize yote na apate kujenga nyumba hii ya utukufu niliyoifanyia matayarisho.”


Unijaze furaha na shangwe, unifurahishe tena, mimi ambaye uliniponda.


Nimekukosea wewe peke yako, nimetenda mabaya mbele yako. Hivi uamuzi wako ni wa haki, hukumu yako haipotoki.


Zaburi ya Asafu. Hakika, Mungu ni muzuri kwa Israeli, kwa watu wenye moyo safi.


Maana walinzi wa Israeli wote ni vipofu; wote hawana akili yoyote. Wote ni kama imbwa bubu wasioweza kufoka, wanalala tu na kuota ndoto, wanapenda sana kusinzia!


Kwa hiyo, Yawe hawahurumii vijana wao, hana huruma juu ya wayatima na wajane wao; maana hakuna hata mumoja anayemufuata, kila mutu anasema upumbafu. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Kisha siku hizo, nitafanya agano hili na Waisraeli. Nitaiweka sheria yangu ndani yao, na kuiandika katika mioyo yao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Nitawapa moyo mupya na kuweka roho mupya ndani yenu. Nitauondoa ule moyo mugumu kama jiwe na kuwapa moyo musikilivu,


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


Muwaache! Wao ni vipofu, wanaongoza vipofu wengine. Na kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili wanatumbukia ndani ya shimo.”


Yesu akawajibu: “Munadanganyika, kwa sababu ya kutojua Maandiko Matakatifu wala uwezo wa Mungu.


Nyuma ya siku tatu, wakamukuta ndani ya hekalu, akiikaa katikati ya walimu wakubwa wa Sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maulizo.


Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Wafarisayo na walimu wakubwa wa Sheria waliotoka katika kila kijiji cha jimbo la Galilaya na la Yudea na toka Yerusalema, walikuwa wakiikaa pale. Naye alikuwa akiponyesha wagonjwa kwa uwezo wa Bwana.


Basi Nikodemo akamwuliza: “Maneno haya yanawezekana namna gani?”


Lakini Mufarisayo mumoja, jina lake Gamalieli, aliyekuwa mwalimu wa Sheria na aliyeheshimiwa sana na watu wote, akasimama katika baraza na kuamuru mitume wapelekwe inje kwa muda.


Kwa maana kuonekana kwa inje kwa Muyuda si kuwa Muyuda wa kweli, wala kutahiriwa kimwili tu si kutahiriwa kwa kweli.


Kwa hiyo, mutahiri magovi ya mioyo yenu, musikuwe wagumu tena.


Yawe, Mungu wenu, atawafanya ninyi na wazao wenu mukuwe na moyo wa utii kusudi mumupende yeye kwa moyo wenu wote na roho yenu, mupate kuishi.


Sisi ndio wenye kutahiriwa kwa kweli, maana tunamwabudu Mungu kwa uongozi wa Roho wake na kujivuna kwa ajili ya Yesu Kristo. Sisi hatuweki tumaini letu katika mambo ya kimwili.


Katika kuungana naye, mumetahiriwa wala si kwa mikono ya watu, lakini mumetahiriwa na Kristo, na kutahiriwa kule kumewakomboa toka katika hali zaifu ya kimwili.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ