Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 21:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Akamwuliza tena mara ya pili: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Naye akamujibu: “Ndiyo, Bwana, unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia tena: “Chunga kondoo wangu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 21:16
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mujue kwamba Yawe ndiye Mungu. Yeye ndiye aliyetuumba, sisi ni mali yake; sisi ni watu wake na kondoo wake anaowachunga.


Maana yeye ni Mungu wetu. Sisi ni watu wake, kondoo wanaochungwa katika malisho yake. Heri leo mungesikiliza hivi anavyosema:


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


‘Ewe Betelehemu, katika inchi ya Yuda, wewe si mudogo kabisa kati ya miji mikubwa ya Yuda, maana ndani yako atatoka mutawala, atakayechunga watu wangu, ndio Waisraeli.’ ”


Mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atayatenga kwa makundi mawili kama vile muchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi.


Lakini Petro akakana tena akaapa akisema: “Ninaapa ya kuwa simujui mutu huyu!”


Kwa maana Mwana wa Mutu alikuja kutafuta na kuokoa yule aliyepotea.”


Yule mwanamuke akamwambia Petro: “Wewe vilevile si mumoja wa wanafunzi wa mutu huyu?” Petro akamujibu: “Hapana! Mimi si mwanafunzi wake.”


Wakati ule Simoni Petro alikuwa angali pale akiota moto. Basi wakamwuliza: “Wewe vilevile si mumoja wa wanafunzi wa mutu huyu?” Petro akakana, akisema: “Hapana! Mimi si mwanafunzi wake.”


Kisha Yesu akamwuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Basi Petro akauzika kwa sababu Yesu alimwuliza mara ya tatu kama anamupenda. Kwa hiyo akamujibu: “Bwana, unajua yote; unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza kondoo wangu.


Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.


Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,


Kwa maana mulikuwa kama kondoo wanaopotea, lakini sasa mumerudi kwa yule anayekuwa muchungaji na mwangalizi wa roho zenu.


Ninawaonya, muchunge lile kundi Mungu alilowapatia, si kwa kulazimishwa, lakini kwa mapenzi yenu sawa vile Mungu anavyotaka. Musitumike kwa ajili ya tamaa mbaya ya mali, lakini kwa kujitoa kwa moyo mwema.


Kwa maana Mwana-Kondoo anayekuwa katikati ya kiti cha kifalme, atawachunga na kuwaongoza kwenye chemichemi ya maji ya uzima. Naye Mungu atawapanguza machozi yao yote.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ