Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 21:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Walipokwisha kula, Yesu akamwuliza Simoni Petro: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda mimi kuliko hawa?” Naye akamujibu: “Ndiyo, Bwana, unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza wana-kondoo wangu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 21:15
49 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Yakobo akamwambia: “Bwana wangu, wewe unajua kwamba watoto hawa ni wachanga, na kwamba nyama hawa wananyonyesha, nami ninapaswa kuwatunza. Kama nyama hawa watapelekwa mbio kwa siku moja, wote watakufa.


Nikuambie nini zaidi, mimi Daudi? Maana wewe unanijua mimi mutumishi wako, ee Bwana wangu Yawe!


“Ee Yawe, ninakusihi ukumbuke jinsi nilivyokutumikia kwa uaminifu na kwa moyo wangu wote na kutenda mazuri mbele yako.” Hezekia akalia kwa uchungu sana.


Atachunga kundi lake kama muchungaji, atawakusanya wana-kondoo katika mikono yake, atawabeba kwa kifua chake, na atawaongoza polepole kondoo wanaonyonyesha.


Nitawapa wachungaji watakaowatunza vema, nao hawatakuwa na woga tena wala kufazaika, na hakuna hata mumoja wao atakayepotea. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nitawapa wachungaji wanaopendeza moyo wangu, watakaowakulisha kwa akili.


Nitaweka muchungaji mumoja juu yao, mufalme kama mutumishi wangu Daudi. Yeye atawakulisha na kuwa muchungaji wao.


Yule mutu akaniambia: Haya ni mafika ambako watumishi wa nyumba ya Yawe watapikia sadaka watu wanazoleta.


“Yeye anayemupenda baba yake au mama yake kuliko mimi, hastahili kuwa wangu, na yeyote anayemupenda mwana wake au binti yake kuliko mimi hastahili kuwa wangu vilevile.


Halafu Yesu akamwambia: “Heri kwako, wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana hakuna mutu aliyekufunulia neno hili isipokuwa Baba yangu anayekuwa mbinguni.


“Mufanye angalisho, musimuzarau mumoja wa hawa wadogo; kwa sababu ninawaambia kwamba wamalaika wao wanaokuwa mbinguni wako siku zote karibu na Baba yangu anayekuwa mbinguni. [


Petro akamujibu: “Hata wote wakianguka, mimi sitaanguka hata kidogo.”


Lakini Petro akamwambia: “Hata ikinipasa kufa pamoja nawe, sitakukana hata kidogo.” Na wanafunzi wote wengine wakasema sawasawa naye.


Petro akamwambia: “Hata wote wengine wakianguka, mimi sitaanguka.”


“Musiogope ninyi kundi dogo! Kwa kuwa Baba yenu amependelea kuwapa ninyi ule Ufalme wake.


Lakini mimi nimekuombea, kusudi usipungukiwe na imani. Nawe utakaponirudilia tena, uwatie wandugu zako moyo.”


Kisha akamupeleka Simoni kwa Yesu. Yesu akamwangalia, akasema: “Wewe ndiwe Simoni mwana wa Yoane, sasa utaitwa Kefa.” (Jina “Kefa” ni sawasawa na “Petro” na maana yake ni “Jiwe.”)


Petro akamwuliza: “Bwana, sababu gani siwezi kukufuata sasa? Mimi ni tayari kutoa maisha yangu kwa ajili yako!”


kwa maana Baba mwenyewe anawapenda. Anawapenda ninyi kwa sababu mumenipenda na kuamini kwamba nilitoka kwa Mungu.


Yesu akawaambia: “Mukuje mukule.” Na hakuna hata mumoja kati ya wanafunzi aliyesubutu kumwuliza kwamba yeye ni nani, kwa maana walijua kwamba ni Bwana.


Halafu mwanafunzi yule aliyependwa na Yesu akamwambia Petro: “Ni Bwana.” Simoni Petro aliposikia kwamba ni Bwana, akavaa kanzu yake (kwa maana alikuwa havai kitu), naye akajitupa ndani ya maji.


Yesu akawaambia: “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mungenipenda, kwa maana nimetoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikukuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini yeye ndiye aliyenituma.


Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.


Ninajua kwamba nyuma ya kuondoka kwangu, imbwa wakali wa pori wataingia katikati yenu, nao hawatahurumia kundi lile.


Mumupokee yule anayekuwa zaifu katika imani pasipo kubishana naye juu ya mawazo yake.


Sisi tunaokuwa na nguvu katika imani tunapaswa kubeba muzigo wa uzaifu wa wale wasiokuwa na nguvu. Tusifanye tu mambo yanayotupendeza wenyewe.


Na hivi kwa sababu ya elimu yako, yule ndugu mwamini zaifu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake, atapotea.


Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.


Basi, hatutakuwa tena kama watoto, tukipeperushwa na kuvutwa na mafundisho ya kila aina yanayoletwa na watu wanaodanganya wengine na kuwapotosha kwa mayele yao.


Ninawatakia neema wale wote wanaomupenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usiokuwa na mwisho.


Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,


Hakuna kitu kinachoweza kufichwa mbele ya Mungu, lakini vitu vyote vinafunuliwa na viko wazi mbele ya macho yake, yeye tutakayemutolea hesabu ya maneno yetu.


Ninyi munamupenda ijapokuwa hamujamwona, na munamwamini ijapokuwa sasa hamumwoni. Na zaidi ya ile munashangilia kwa furaha isiyoweza kuelezwa, inayojaa utukufu,


Kama vile watoto wachanga wanaotamani maziwa, na ninyi vilevile mukuwe na hamu ya kunywa maziwa safi ya kiroho, kusudi mupate kukomaa na kuokolewa.


Kwa maana mulikuwa kama kondoo wanaopotea, lakini sasa mumerudi kwa yule anayekuwa muchungaji na mwangalizi wa roho zenu.


Sisi tuko na upendo kwa sababu Mungu ndiye aliyetupenda wa kwanza.


Mutu yeyote anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo, yeye ni mutoto wa Mungu; na kila mutu anayemupenda baba anamupenda mwana wake vilevile.


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ