Yoane 21:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Yesu akawaambia: “Mukuje mukule.” Na hakuna hata mumoja kati ya wanafunzi aliyesubutu kumwuliza kwamba yeye ni nani, kwa maana walijua kwamba ni Bwana.
Yesu alitambua kwamba walitaka kumwuliza. Basi akawaambia: “Munaulizana juu ya maneno niliyosema kwamba kunabaki wakati kidogo nanyi hamutaniona, lakini kisha wakati kidogo mutaniona tena?
Basi Simoni Petro akapanda ndani ya chombo, akakokota wavu mpaka inchi kavu. Nao ulikuwa umejaa samaki wakubwa mia moja makumi tano na tatu. Na ijapokuwa walikuwa wengi vile, wavu haukupasuka.
Saa ile ile wanafunzi wa Yesu wakarudi, nao wakashangaa kumwona akisemezana na mwanamuke. Lakini hakuna mumoja wao aliyemwuliza yule mwanamuke kwamba anataka nini au kumwuliza Yesu kwamba sababu gani anasema naye.