Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 20:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Kisha akamwambia Toma: “Ujongeze kidole chako hapa na uione mikono yangu; unyooshe mukono wako na kugusa ndani ya ubavu wangu. Usikuwe tena na mashaka, lakini uamini.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 20:27
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Mungu mwenye huruma alisamehe uovu wao, wala hakuwaangamiza. Mara nyingi alizuia hasira yake, wala hakuacha kasirani yake yote iwake.


Na Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu na chenye kupotoka. Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”


Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu! Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”


Muangalie mikono yangu na miguu yangu, kusudi mupate kutambua kwamba ni mimi. Muniguse, muone, kwa maana muzimu hana mwili wala mifupa kama hivi munavyoniona kuwa navyo.”


Alipokwisha kusema vile, akawaonyesha mikono na miguu yake.


Na Yesu akajibu: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu na chenye kupotoka! Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Umulete mutoto wako hapa.”


Kisha kusema hivi, Yesu akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi wanafunzi wakafurahi wakati walipomwona Bwana.


Wanafunzi wengine wakamwambia: “Tumemwona Bwana.” Lakini Toma akawajibu: “Nisipoona alama za misumari katika mikono yake na kutia kidole changu katika kovu za misumari ile, nami nisipoingiza vidole vyangu ndani ya ubavu wake, sitaamini.”


Toma akamujibu: “Bwana wangu na Mungu wangu!”


Sheria ilitokea na kusababisha kuongezeka kwa makosa, lakini nafasi yoyote palipozidi zambi, neema ilizidi sana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ