Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 20:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Alipokwisha kusema maneno haya, akawapulizia pumzi na kuwaambia: “Mupokee Roho Mutakatifu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 20:22
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yawe Mungu akamwumba mwanaume kwa udongo, akamupulizia ndani ya pua pumzi ya uzima, na yule mwanaume akakuwa kiumbe chenye uzima.


Roho ya Mungu iliniumba, nayo pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo inanipa uzima.


Mbingu ziliumbwa kwa neno la Yawe, na vyote vinavyokuwa ndani yake kwa pumzi ya kinywa chake.


Halafu, Yawe akaniambia: Ewe mwanadamu, kwa ajili yangu toa unabii kwa upepo, uuambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ewe upepo kuja toka pande zote ine na kuipulizia miili hii iliyokufa kusudi ipate kuishi.


Nami nitamwomba Baba awape musaidizi mwingine kwa kukaa nanyi milele;


“Wakati Musaidizi nitakayewatumia toka kwa Baba atakapokuja, atanishuhudia mimi. Yeye ni Roho wa ukweli, naye anakuja toka kwa Baba.


Lakini mimi ninawaambia ukweli: ni faida kwenu mimi niende, kwa maana nisipokwenda, Musaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, nitamutuma kwenu.


Yesu akawaambia tena: “Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma, mimi ninawatuma ninyi vilevile.”


Watu wote mutakaowasamehe zambi, watasamehewa; nao wote musiowasamehe, hawatasamehewa.”


(Alisema vile juu ya Roho atakayepokelewa na wale wanaomwamini Yesu. Kwa wakati ule Roho alikuwa hajatumwa bado, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.)


“Ni nani anayeweza kuwazuiza watu hawa waliopewa Roho Mutakatifu kama sisi wasibatizwe kwa maji?”


akawauliza: “Ninyi mulipokea Roho Mutakatifu wakati mulipoamini?” Nao wakamujibu: “Hapana! Hatujasikia hata kidogo kwamba kuko Roho Mutakatifu.”


Petro akawajibu: “Mugeuke toka katika zambi zenu, na kila mumoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo, na Mungu atawasamehe zambi zenu. Hivi mutapokea zawadi ya Roho Mutakatifu.


Wote wakapewa Roho Mutakatifu na kuanza kusema kwa luga mbalimbali kwa kadiri Roho alivyowawezesha kusema.


Halafu Petro akiwa amejazwa na Roho Mutakatifu, akawajibu: “Ninyi wasimamizi wa watu, nanyi wazee:


Walipofika Samaria, wakawaombea waamini wapate kupokea Roho Mutakatifu.


Ninataka mujibu ulizo hili moja: mumepokea Roho wa Mungu kwa sababu ya kushika Sheria au kwa sababu mumesikia na kuamini Habari Njema?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ