Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 20:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Magaribi ya ile ile siku ya kwanza ya juma, wanafunzi walikusanyika katika nyumba na milango ilikuwa imefungwa, kwa sababu waliwaogopa wakubwa wa Wayuda. Mara moja Yesu akawatokea na kusimama katikati yao, akawaambia: “Amani kwenu!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 20:19
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa ajili ya jamaa na wandugu zangu, ee Yerusalema, ninakutakia amani!


Kama watu wa nyumba ile wakiwakaribisha, wakuwe na amani ile muliyowatakia, lakini wasipowakaribisha, amani ile iwarudilie.


Kwa maana pahali popote watu wawili au watatu wanapokusanyika kwa ajili ya jina langu, mimi ni pale katikati yao.”


Kwa mwisho Yesu akawatokea wanafunzi kumi na mumoja walipokuwa wakikula. Naye akawakaripia kwa sababu ya kutokuamini kwao na kwa sababu ya ugumu wao. Kwa maana hawakusadikia wale waliomwona nyuma ya kufufuka kwake.


“Ninawaachia amani; ninawapa amani yangu. Siwapatii ninyi amani hii kama dunia inavyoitoa. Musifazaike wala musiogope.


Na sasa ninyi vilevile munasikia uchungu, lakini nitawaona tena, nanyi mutafurahi, wala hakuna mutu atakayeweza kuwahuzunisha tena.


Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”


Yesu akawaambia tena: “Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma, mimi ninawatuma ninyi vilevile.”


Ilipotimia juma moja nyuma ya pale, wanafunzi wa Yesu wakakusanyika tena ndani ya nyumba ile ile, na mara hii Toma alikuwa pamoja nao. Ijapokuwa milango ilikuwa imefungwa, Yesu akawatokea tena, akasimama katikati yao na kusema: “Amani kwenu!”


Nyuma ya mambo hayo, Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kandokando ya ziwa la Tiberia. Angalia sasa namna alivyowatokea:


Hii ndiyo mara ya tatu Yesu aliyowatokea wanafunzi wake tangu alipofufuka.


Lakini hakuna mutu aliyesema juu yake waziwazi, kwa sababu waliwaogopa wakubwa wa Wayuda.


Nyuma ya kufa kwake, alijionyesha kwao kwa namna nyingi kwa kuhakikisha kwamba amefufuka. Kwa muda wa siku makumi ine, alionekana kwao na kusema nao juu ya maneno yanayoelekea Ufalme wa Mungu.


Basi Mungu anayeleta amani akuwe pamoja nanyi wote. Amina!


Alimutokea Petro, na kisha akawatokea mitume wake kumi na wawili.


Kwa maana Kristo mwenyewe ndiye aliyetuletea amani akifanya Wayuda na watu wa mataifa mengine kuwa jamii moja. Kwa njia ya kutoa mwili wake, amevunja uadui uliokuwa kama ukuta uliowatenganisha.


Ninawatakia wandugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kwa Bwana Yesu Kristo.


Tunawatakia neema na amani toka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo.


Bwana wa amani mwenyewe awape amani siku zote na kwa njia zote. Bwana akuwe pamoja nanyi wote.


naye Abrahamu akamupa fungu moja la kumi la vitu vyote alivyoteka. Maana ya jina la Melkisedeki, kwanza ni “Mufalme wa haki,” tena ni mufalme wa Salemu, ni kusema “Mufalme wa amani.”


Ninatumaini kwamba nitakuona sasa hivi na wakati ule tutasemezana pamoja uso kwa uso.


Ni mimi Yoane ninayewaandikia ninyi makanisa saba munaokuwa katika jimbo la Azia. Ninawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu anayekuwa, aliyekuwa na anayekuja, na kutoka kwa roho saba wanaokuwa mbele ya kiti chake cha kifalme,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ