Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 20:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Siku ya kwanza ya juma asubui mapema, kulipokuwa kungali giza, Maria wa Magdala akaenda kwenye kaburi. Alipofika kule akaona kama jiwe lililofunika kaburi limeondolewa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 20:1
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kati yao kulikuwa Maria wa Magdala, Maria mama ya Yakobo na Yosefu, pamoja na mama ya wana wa Zebedayo.


Akaiweka ndani ya kaburi lake jipya alilojichimbia katika jiwe. Kisha akasukumia jiwe kubwa kwenye kiingilio cha lile kaburi na kujiendea.


Basi uamuru kaburi lichungwe mpaka zile siku tatu nyuma ya kufa kwake zitakapotimia, kusudi wanafunzi wake wasifike kuiba maiti yake na kuwaambia watu kwamba amefufuka.”


Basi wakaenda, wakatia muhuri juu ya lile jiwe, na wakaweka waaskari pale kwa kulichunga.


Siku ya Sabato ilipokwisha kupita, kesho yake siku ya kwanza ya juma, kwa wakati wa mapambazuko, Maria wa Magdala na Maria mwingine wakaenda kuangalia kaburi.


Kwa rafla kukatokea tetemeko la inchi, kwa maana malaika wa Bwana alishuka toka mbinguni, akasukuma lile jiwe lililofunga kaburi pembeni na kuikaa juu yake.


Yosefu akanunua vitambaa, akaondoa maiti ya Yesu juu ya musalaba, akaifungafunga na vile vitambaa na kuiweka ndani ya kaburi lililochimbwa ndani ya jiwe. Kisha wakasukumia jiwe kwenye kiingilio cha lile kaburi.


Yesu alipokwisha kufufuka asubui mapema, siku ya kwanza ya juma, alimutokea kwanza Maria wa Magdala, yule aliyefukuza pepo saba toka ndani yake.


Basi Yesu akasisimua tena kwa huzuni, na kwenda kwenye kaburi. Kaburi lile lilikuwa pango lililofungwa na jiwe kubwa.


Basi wakaondosha lile jiwe. Yesu akainua macho juu, akasema: “Baba, ninakushukuru kwa sababu umenisikia.


Mama ya Yesu, dada ya mama yake, Maria muke wa Kleopa na Maria wa muji wa Magdala walikuwa wamesimama karibu na musalaba wake.


Ilipotimia juma moja nyuma ya pale, wanafunzi wa Yesu wakakusanyika tena ndani ya nyumba ile ile, na mara hii Toma alikuwa pamoja nao. Ijapokuwa milango ilikuwa imefungwa, Yesu akawatokea tena, akasimama katikati yao na kusema: “Amani kwenu!”


Siku ya kwanza ya juma, tulikuwa tunakusanyika kwa kumega mukate. Paulo akasemezana na watu na kuendelea kuwahubiria mpaka katikati ya usiku, kwa sababu alikusudia kuondoka kesho yake.


Kila siku ya kwanza ya juma, kila mumoja wenu anapaswa kuweka akiba ya mali kwake, kwa kadiri ya mapato yake, kusudi musihitaji kufanya muchango wakati nitakapokuja.


Siku moja ya kumwabudu Bwana, nikashikwa na Roho wa Mungu, nikasikia sauti kubwa, inayolia kama baragumu,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ