Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Lakini Yesu akamujibu: “Mama, kuna maneno gani kati yako nami? Saa yangu haijatimia bado.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 2:4
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini mufalme akamwambia: “Kuna maneno gani kati yangu na ninyi wana wa Zeruya? Ikiwa Yawe amemwambia: ‘Umulaani Daudi’, nani sasa anaweza kuuliza: ‘Kwa nini umefanya hivyo?’ ”


Halafu Abisayi mwana wa Zeruya akasema: “Si Simei anapaswa kuuawa maana alimulaani muchaguliwa wa Yawe?”


Yule mwanamuke akamwambia Elia: “Ewe mutu wa Mungu, kuna maneno gani kati yako nami? Kumbe ulikuja kwangu kwa kuzifichua zambi zangu na kusababisha kifo cha mwana wangu?”


Kuna muda kwa kila kitu, na wakati kwa kila jambo katika dunia:


Halafu Yesu akamujibu: “Wewe mwanamuke, imani yako ni kubwa! Ifanyike kwako sawa ulivyoomba.” Na binti yake akapona tangia saa ile ile.


Halafu wakaanza kulalamika wakisema: “Kuna maneno gani kati yako na sisi wewe Mwana wa Mungu? Umekuja hapa kwa kututesa mbele ya kutimia kwa wakati wetu?”


Yesu akawajibu: “Kwa nini mulinitafuta? Hamujui kwamba ninapaswa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”


Yesu akawajibu: “Saa ya kutukuzwa kwa Mwana wa Mutu imetimia.


Kulikuwa kumebaki siku moja mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kutoka katika dunia na kurudi kwa Baba yake imetimia. Yeye alikuwa akiwapenda watu wake waliokuwa katika dunia, na akaendelea kuwapenda mpaka mwisho.


Wakati divai ilipomalizika, mama ya Yesu akamwambia: “Hawana divai tena.”


Wale wamalaika wakamwuliza: “Ee mama, kwa sababu gani unalia?” Naye akawajibu: “Kwa sababu wameondoa maiti ya Bwana, nami sijui pahali walipoiweka.”


Yesu akamwuliza: “Mama, kwa sababu gani unalia? Unamutafuta nani?” Maria akizani kwamba ni mulimaji wa bustani, akamwambia: “Bwana, kama ni wewe uliyeondoa maiti yake, uniambie pahali ulipoiweka, nami nitakwenda kuitwaa.”


Basi wakatafuta kumufunga, lakini hakuna mutu aliyemukamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijatimia.


Na Yesu akawaambia: “Wakati unaofaa kwangu haujatimia; lakini wakati wowote unafaa kwenu.


Ninyi muende kwa sikukuu. Mimi sijaenda bado kwa sikukuu hii, kwa sababu wakati unaofaa kwangu haujatimia.”


Yesu alisema maneno haya wakati alipokuwa akifundisha katika hekalu, kwenye sanduku za kuwekea matoleo. Hakuna mutu aliyemufunga, kwa sababu wakati wake ulikuwa haujatimia.


Kwa hiyo basi, tangu sasa hatumuhesabu tena mutu yeyote kufuatana na hali ya kimutu. Hata ikiwa tulimuhesabu Kristo kufuatana na hali ya kimutu, kwa sasa hatumuhesabu tena kufuatana na hali ile.


Walawi waliacha wazazi wao, wakawasahau wandugu zao, hawakuwatambua hata watoto wao, maana walifuata amri zako, na kushika agano lako.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ