Wakubwa wake wakaibeba maiti yake katika gari na kuirudisha Yerusalema walikomuzika katika kaburi lake mwenyewe. Kisha watu wa Yuda wakamuchukua Yoahazi mwana wa Yosia, wakamupakaa mafuta na kumuweka kuwa mufalme kwa pahali pa baba yake.
Alipokwisha kuishusha toka juu ya musalaba, akaifungafunga na vitambaa na kuiweka ndani ya kaburi lililochimbwa katika jiwe. (Ndani ya kaburi lile mulikuwa bado hamujazikwa mutu.)
Yesu akamwuliza: “Mama, kwa sababu gani unalia? Unamutafuta nani?” Maria akizani kwamba ni mulimaji wa bustani, akamwambia: “Bwana, kama ni wewe uliyeondoa maiti yake, uniambie pahali ulipoiweka, nami nitakwenda kuitwaa.”