Akazikwa katika kaburi alilokuwa amejichimbia yeye mwenyewe, katika muji wa Daudi. Walimulalisha juu ya kitanda kilichokuwa kimejazwa marasi ya kila aina yaliyotayarishwa na wafundi wa kutengeneza marasi, wakawasha moto mukubwa sana kwa heshima yake.
Lakini Petro alisimama, akaenda mbio mpaka kwenye kaburi. Alipoinama kuchungulia ndani yake, akaona tu vile vitambaa. Kisha akarudia kwake, akishangaa kwa ajili ya mambo yaliyotokea.
Halafu yule marehemu akatoka inje, akiwa amefungwa mikono na miguu kwa vitambaa, na uso wake ukifunikwa na nguo. Yesu akawaambia: “Mumufungue, mumwache ajiendee.”