Yoane 19:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
4 Pilato akatoka tena inje na kuwaambia Wayuda: “Angalia, nitawaletea naye hapa inje kusudi mupate kujua kwamba mimi sioni hata sababu moja ya kumuhukumu.”
Pilato alipokuwa amekwisha kuikaa kwa kuamua maneno, muke wake akamutumia ujumbe huu: “Usijiingize katika maneno ya mutu huyo mwenye haki, kwa sababu usiku niliteseka sana katika ndoto kwa ajili yake.”
Basi Pilato alipoona kwamba hataweza kufanya kitu, isipokuwa tu kuongeza fujo, akatwaa maji na kunawa mikono yake mbele ya watu wote, akisema: “Lazima ya damu ya mutu huyu isikuwe juu ya kichwa changu! Maneno haya yanawaangukia.”
Mukubwa wa waaskari na wale waliokuwa pamoja naye wakimuchunga Yesu walipoona tetemeko la inchi na mambo yote yaliyofanyika, wakaogopa sana, na kusema: “Hakika mutu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
Pilato akamwuliza: “Ukweli ni nini?” Pilato alipokwisha kusema neno hili, akatoka tena inje na kuwaambia Wayuda: “Mimi sioni hata sababu moja ya kumuhukumu mutu huyu.
Basi wakati wale wakubwa wa makuhani na walinzi walipomwona, wakapiga kelele, wakisema: “Umutundike juu ya musalaba! Umutundike juu ya musalaba!” Pilato akawaambia: “Mumutwae ninyi wenyewe na kumutundika, kwa maana mimi sioni sababu ya kumuhukumu.”
Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.
Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.