Akazikwa katika kaburi alilokuwa amejichimbia yeye mwenyewe, katika muji wa Daudi. Walimulalisha juu ya kitanda kilichokuwa kimejazwa marasi ya kila aina yaliyotayarishwa na wafundi wa kutengeneza marasi, wakawasha moto mukubwa sana kwa heshima yake.
Wakaingia ndani ya nyumba, wakamwona mutoto pamoja na mama yake, Maria. Wakapiga magoti na kumwabudu mutoto. Kisha wakafungua mizigo yao na kumutolea zawadi ya zahabu, ubani na marasi.
Siku ya Sabato ilipokwisha kupita, Maria wa Magdala, na Maria mama ya Yakobo, na mwanamuke mwingine Salome, walinunua marasi kusudi waende kupakaa maiti ya Yesu.
Halafu Maria akatwaa nusu ya litre ya marasi ya bei kali, yaliyotengenezwa na maua ya nardo safi. Akaipakaa kwa miguu ya Yesu na kuipanguza na nywele zake. Nyumba yote ikajaa harufu ya marasi.