Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 19:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Siku ile ilikuwa ya matayarisho ya siku ya Sabato iliyofuata. Kwa sababu hii Wayuda hawakutaka maiti za wale waliotundikwa zibaki juu ya misalaba kwa maana siku ile ilikuwa kubwa sana. Kwa hiyo wakamwomba Pilato ruhusa kwamba miguu ya wale waliotundikwa ivunjwe kusudi wakufe mbio na maiti zao ziondoshwe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 19:31
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku ya kwanza na siku ya saba mutakuwa na mukutano mutakatifu. Katika siku hizo mbili hamutaruhusiwa kufanya kazi yoyote isipokuwa kazi ya lazima ya kutayarisha chakula.


Mutu mwenye haki anajali nyama wake, lakini huruma za waovu ni kutesa tu.


Munajikulisha kwa nyama ya watu wangu, munawachuna ngozi yao, munaivunjavunja mifupa yao, na kuwakatakata kama nyama ya kupika, kama nyama ya kutia ndani ya chungu.


Kesho yake, maana yake siku iliyofuata ile ya matayarisho ya siku ya Sabato, wakubwa wa makuhani na Wafarisayo wakamwendea Pilato,


Ilipokwisha kuwa magaribi, Yosefu wa Arimatea, akafika kwa Pilato. (Yosefu alikuwa mutu mwenye heshima katika Baraza Kubwa, na vilevile alikuwa akitazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu). Siku ile ilikuwa ya matayarisho ya siku ya Sabato iliyofuata. Kwa hiyo Yosefu akaenda bila woga kwa Pilato kwa kumwomba maiti ya Yesu.


Halafu Pilato akaamuru wamukamate Yesu na kumupiga fimbo.


Siku ile ilikuwa siku ya matayarisho ya Pasaka, karibu na saa sita. Pilato akawaambia Wayuda: “Mufalme wenu huyu!”


Na kwa kuona siku ile ilikuwa ya matayarisho ya siku ya Sabato ya Wayuda na kaburi lilikuwa karibu, wakamuzika Yesu mule.


Kisha akamutundika mufalme wa Ai juu ya muti wa tini mpaka magaribi. Lakini jua lilipoanza kutua, Yoshua aliamuru maiti yake iondolewe juu ya muti na kutupwa kwenye mulango wa muji kisha walundike lundo kubwa la mawe juu ya maiti hiyo. Lundo hilo liko kule mpaka leo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ