3 Wakafika kila wakati mbele yake na kusema: “Jambo, Mufalme wa Wayuda.” Nao wakamupiga makofi.
Yuda alipofika, akamujongelea Yesu, na kumwambia: “Jambo, Mwalimu.” Na kisha akamubusu.
Nao wakasokota taji na tawi lenye miiba na kumuvalisha nalo kwenye kichwa chake. Wakaweka tete katika mukono wake wa kuume, wakapiga magoti mbele yake na kumuchekelea, wakisema: “Jambo, Mufalme wa Wayuda!”
Kisha wakaanza kumusalimia, wakisema: “Jambo, Mufalme wa Wayuda!”
Malaika akamufikia kwenye nyumba yao na kumwambia: “Salamu kwako, wewe uliyejaliwa neema kutoka kwa Mungu! Bwana yuko pamoja nawe.”
Yesu aliposema maneno haya, mumoja wa walinzi waliokuwa karibu naye, akamupiga kofi, akisema: “Ni hivi unavyopaswa kumujibu Kuhani Mukubwa?”
Halafu Pilato akarudi ndani ya nyumba, akamwita Yesu na kumwuliza: “Wewe ni mufalme wa Wayuda?”