Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 19:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Pale kulikuwa chombo chenye kujaa divai yenye kuchacha. Basi waaskari wakachovya kikausho ndani ya ile divai, wakakifungia juu ya tawi la hisopo na kukiweka kwa kinywa chake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 19:29
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mimi ni mukosaji tangia kuzaliwa kwangu, mwenye zambi tangia tumbo la mama yangu.


Mutatwaa majani ya hisopo na kuyachovya katika damu ndani ya beseni na kupakaa vizingiti na miimo yote miwili ya milango ya nyumba zenu. Mutu yeyote asitoke inje ya nyumba usiku ule mpaka asubui.


Mutu anayekuwa safi atatwaa hisopo, halafu ataichovya katika maji hayo, kisha atainyunyizia hema, vyombo vyote vinavyokuwa ndani ya hema na watu wanaokuwa ndani. Atamunyunyizia vilevile mutu aliyegusa mufupa wa mutu, au mwili wa mutu aliyeuawa au aliyekufa kifo cha kawaida, au aliyegusa kaburi.


wakamupa Yesu divai iliyochanganywa na kinywaji chenye uchungu sana. Lakini alipoionja, akakataa kuikunywa.


Mara moja, mumoja wao akaenda mbio akatwaa kikausho, akakichovya ndani ya divai yenye kuchacha. Akakifungia juu ya tete, akakipandishia Yesu, kusudi apate kunywa.


Lakini Yesu, akalalamika tena kwa sauti kubwa na kukata roho.


Na mumoja wao akaenda mbio, akachovya kikausho ndani ya divai yenye kuchacha na kukifungia juu ya tete. Kisha akakipandishia Yesu, kusudi apate kunywa, akisema: “Mwache tuone kama Elia atakuja kumushusha juu ya musalaba.”


Waaskari vilevile walimuzarau, wakamupelekea divai yenye kuchacha


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ