Yoane 19:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
20 Pahali pale Yesu alipotundikwa palikuwa karibu na muji, kwa hiyo Wayuda wengi walisoma andiko lile. Nalo lilikuwa limeandikwa katika Kiebrania, Kilatini na Kigriki.
Pilato aliposikia maneno haya, akamupeleka Yesu inje; akaikaa katika kiti cha hukumu kwenye nafasi inayoitwa katika Kiebrania “Gabata,” maana yake “Sakafu ya Mawe.”
Kule Yerusalema, karibu na mulango wa muji huu unaoitwa “Mulango wa Kondoo,” kuna kisima chenye viingilio vitano vyenye paa. Kisima kile kinaitwa katika Kiebrania “Betesaida.”
Waaskari walipotaka kumwingiza Paulo katika upango, akamwuliza mukubwa wa kundi la waaskari: “Unaweza kuniruhusu kukuambia neno moja?” Yule mukubwa wa kundi la waaskari akamwuliza: “Unajua Kigriki?
Yule mukubwa wa kundi la waaskari akamuruhusu. Basi Paulo akasimama juu ya ngazi, akainua mukono kwa kuwaalika watu wanyamaze. Na watu waliponyamaza kabisa, Paulo akawaambia maneno haya katika luga ya Kiebrania:
Sisi wote tukaanguka chini, na nikasikia sauti iliyoniambia hivi katika luga ya Kiebrania: ‘Saulo, Saulo, kwa sababu gani unanitesa? Unajiumiza bure kama ngombe anayepiga teke kwenye chongo ya fimbo ya mwenyeji wake.’
Na mufalme wao, ndiye malaika wa lile shimo ndefu la kuzimu, jina lake liliitwa kwa Kiebrania “Abidani” na kwa kigriki “Apolioni” (maana yake “Mwangamizaji”).