Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 18:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Wakamujibu: “Yesu wa Nazareti.” Yesu akawaambia: “Ni mimi.” Na Yuda, yule aliyekuwa amemutoa, alikuwa akisimama pale pamoja nao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 18:5
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ubaguzi wao unashuhudia juu yao; wanatangaza zambi yao kama vile watu wa Sodoma, wala hawaifichi. Ole kwao watu hao, kwa sababu wamejiletea maangamizi wenyewe.


Walisikia haya walipotenda machukizo hayo? Hapana, hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo, wataanguka pamoja na wale walioanguka; nitakapowaazibu, wataangamia. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Kule akakaa katika muji ulioitwa Nazareti, kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa mutu wa Nazareti.”


Kundi la watu wakajibu: “Huyu ni nabii Yesu wa Nazareti katika Galilaya.”


Natanaeli akamwuliza: “Kuna kitu kizuri kinachoweza kutoka Nazareti?” Filipo akamujibu: “Kuja uone.”


Basi Yesu akiwa mwenye kujua maneno yote yatakayomupata, akawaendea na kuwauliza: “Munamutafuta nani?”


Yesu alipowaambia: “Ni mimi,” wakarudi nyuma na kuanguka.


Pilato akaamuru andiko liandikwe na kuwekwa juu ya musalaba. Nalo liliandikwa hivi: “Yesu wa Nazareti, Mufalme wa Wayuda.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ