Yoane 18:38 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
38 Pilato akamwuliza: “Ukweli ni nini?” Pilato alipokwisha kusema neno hili, akatoka tena inje na kuwaambia Wayuda: “Mimi sioni hata sababu moja ya kumuhukumu mutu huyu.
Basi Pilato alipoona kwamba hataweza kufanya kitu, isipokuwa tu kuongeza fujo, akatwaa maji na kunawa mikono yake mbele ya watu wote, akisema: “Lazima ya damu ya mutu huyu isikuwe juu ya kichwa changu! Maneno haya yanawaangukia.”
Pilato akatoka tena inje na kuwaambia Wayuda: “Angalia, nitawaletea naye hapa inje kusudi mupate kujua kwamba mimi sioni hata sababu moja ya kumuhukumu.”
Basi wakati wale wakubwa wa makuhani na walinzi walipomwona, wakapiga kelele, wakisema: “Umutundike juu ya musalaba! Umutundike juu ya musalaba!” Pilato akawaambia: “Mumutwae ninyi wenyewe na kumutundika, kwa maana mimi sioni sababu ya kumuhukumu.”