Tungependa ufahamu, ewe mufalme, kwamba Wayuda waliokuja hapa kutoka maeneo mengine ya ufalme wako wamekwenda Yerusalema na wanaujenga upya muji huo wa waasi na waovu. Wanamalizia kujenga kuta zake na kutengeneza musingi.
Na kulipokucha asubui mapema, wakamutosha Yesu kwa Kayafa na kumupeleka kwenye nyumba ya liwali. Lakini Wayuda wenyewe hawakuingia ndani ya nyumba ya liwali, kwa maana kwa njia ile wangejichafua na kutoweza kuwa tayari kula karamu ya Pasaka.
Yesu akajibu: “Ufalme wangu si wa dunia hii. Ufalme wangu ungekuwa wa dunia hii, watumishi wangu wangenipigania kusudi nisitolewe kwa Wayuda. Lakini sasa ufalme wangu si wa hapa katika dunia.”
Yesu akamujibu: “Wewe hauna mamlaka yoyote juu yangu, isipokuwa tu yale uliyopewa na Mungu toka juu. Ni kwa hiyo, yule aliyenitoa kwako anabeba zambi kubwa zaidi.”
Basi wakati wale wakubwa wa makuhani na walinzi walipomwona, wakapiga kelele, wakisema: “Umutundike juu ya musalaba! Umutundike juu ya musalaba!” Pilato akawaambia: “Mumutwae ninyi wenyewe na kumutundika, kwa maana mimi sioni sababu ya kumuhukumu.”
Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa babu zetu, ameonyesha kwamba mutumishi wake Yesu ni mwenye utukufu. Ninyi wenyewe mulimutoa na kumukana mbele ya mutawala Pilato, ijapokuwa Pilato alikuwa ameamua kwamba afunguliwe.