Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 18:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 (Ilifanyika hivi kusudi litimie lile neno Yesu alilosema kwa kuonyesha kifo gani atakachokufa.)

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 18:32
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Koo langu limekauka kama kigae; ulimi wangu unanata ndani ya kinywa changu. Wewe umenilaza pembeni ya kaburi.


na kumutoa katika mikono ya watu wa mataifa mengine. Nao watamuchekelea, watamupiga fimbo na kumutundika juu ya musalaba. Lakini kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.”


“Munajua kwamba kumebaki siku mbili mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mutu apate kutolewa kusudi atundikwe juu ya musalaba.”


Akawaambia: “Tunapanda kwenda Yerusalema na kule Mwana wa Mutu atatolewa kwa wakubwa wa makuhani na kwa walimu wa Sheria. Nao watamuhukumu auawe na kumutoa katika mikono ya watu wa mataifa mengine.


Halafu Wayuda wakaokota tena mawe kwa kumutupia.


Wayuda wakamujibu: “Hatutaki kukutupia mawe kwa ajili ya tendo zuri, lakini kwa sababu unamutukana Mungu. Wewe ni mutu tu, lakini unajifanya kuwa Mungu!”


“Sisemi juu ya ninyi wote; ninawajua wale niliowachagua. Lakini inafaa maneno haya yanayosemwa na Maandiko Matakatifu yatimie: ‘Yule aliyechangia chakula nami, amenigeuka.’


Pilato akawaambia: “Ninyi wenyewe mumukamate na mumuhukumu kufuatana na sheria yenu.” Wakamujibu: “Sisi hatuna ruhusa ya kuua mutu.”


(Yesu alisema maneno haya kwa kuonyesha kifo gani Petro atakachokufa na kumutukuza Mungu.) Kisha kusema maneno haya, Yesu akamwambia: “Unifuate!”


Sawa Musa alivyonyanyua nyoka ya shaba juu ya muti katika jangwa, ni hivi vilevile, sherti Mwana wa Mutu anyanyuliwe,


Halafu Yesu akawaambia: “Wakati mutakapomunyanyua Mwana wa Mutu juu, mutafahamu kwamba ‘Mimi Ndimi.’ Na zaidi ya hii mutatambua kwamba sifanyi neno lolote kwa mapenzi yangu, lakini ninasema tu yale niliyofundishwa na Baba.


Walipokuwa wakimutupia mawe, Stefano akaomba akisema: “Ee Bwana Yesu, pokea roho yangu.”


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


maiti yake isiachwe juu ya muti usiku wote, lakini mutaizika siku hiyohiyo. Maana mutu aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu nanyi hamutachafua inchi yenu muliyopewa na Yawe, Mungu wenu, ikuwe urizi wenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ