Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 18:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Na kulipokucha asubui mapema, wakamutosha Yesu kwa Kayafa na kumupeleka kwenye nyumba ya liwali. Lakini Wayuda wenyewe hawakuingia ndani ya nyumba ya liwali, kwa maana kwa njia ile wangejichafua na kutoweza kuwa tayari kula karamu ya Pasaka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 18:28
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana wao wako mbio kutenda maovu, haraka zao zote ni za kumwanga damu.


Waovu hawalali hata kidogo wasipotenda uovu; hawapati usingizi wasipomukwaza mutu.


Siku ya kumi na ine ya mwezi wa kwanza, mutafanya sikukuu ya Pasaka. Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu.


Ole wao wanaopanga kutenda maovu, wanaolala usiku wakikusudia mabaya! Mara tu kunapopambazuka, wanayatimiza maana wako na uwezo.


Kisha waaskari wa liwali Pilato wakamupeleka Yesu ndani ya upango wa nyumba ya liwali, nalo kundi lao lote wakakusanyika na kumuzunguka.


Waaskari wakamupeleka Yesu ndani ya upango wa nyumba ya liwali, nao wakaita kundi lao lote wakusanyike.


Usiku ulipokucha, wazee wa Wayuda, wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria, wakakusanyika. Wakamuleta Yesu mbele ya Baraza yao Kubwa,


Sikukuu ya Wayuda ya Pasaka ilikuwa karibu. Basi watu wengi toka katika vijiji wakaenda Yerusalema kusudi wajitakase mbele ya Pasaka.


Wakamupeleka kwanza kwa Anasi. Anasi alikuwa mukwe wa Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mukubwa mwaka ule.


Simoni Petro na mwanafunzi mwingine walimufuata Yesu. Yule mwanafunzi alikuwa akijulikana na Kuhani Mukubwa, kwa hiyo akaingia pamoja na Yesu ndani ya upango wa nyumba ya Kuhani Mukubwa.


Halafu Pilato akarudi ndani ya nyumba, akamwita Yesu na kumwuliza: “Wewe ni mufalme wa Wayuda?”


Lakini kufuatana na desturi yenu, ninazoea kuwafungulia mufungwa mumoja wakati wa sikukuu ya Pasaka. Basi munataka niwafungulie mufalme wa Wayuda?”


Yesu akamujibu: “Wewe hauna mamlaka yoyote juu yangu, isipokuwa tu yale uliyopewa na Mungu toka juu. Ni kwa hiyo, yule aliyenitoa kwako anabeba zambi kubwa zaidi.”


Siku ile ilikuwa siku ya matayarisho ya Pasaka, karibu na saa sita. Pilato akawaambia Wayuda: “Mufalme wenu huyu!”


Akaingia tena katika nyumba yake na kumwuliza Yesu: “Wewe ni muzaliwa wa wapi?” Lakini Yesu hakumujibu neno.


Akawaambia: “Ninyi munajua wazi kama katika Sheria ya dini yetu inakatazwa kwa Muyuda kushirikiana na mutu wa taifa lingine wala kumutembelea. Lakini Mungu amenionyesha kwamba haifai kumuhesabia mutu yeyote kuwa muchafu wala mutengwa.


Basi tuma watu waende Yopa kwa kumwita mutu mumoja jina lake Simoni anayeitwa vilevile Petro. Naye anapanga kwa fundi mumoja anayetengeneza vitu vya ngozi anayeitwa Simoni. Nyumba yake iko pembeni ya bahari.’


wakisema: “Uliingia ndani ya nyumba ya watu wasiokuwa wa taifa letu na kula chakula pamoja nao!”


Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa babu zetu, ameonyesha kwamba mutumishi wake Yesu ni mwenye utukufu. Ninyi wenyewe mulimutoa na kumukana mbele ya mutawala Pilato, ijapokuwa Pilato alikuwa ameamua kwamba afunguliwe.


“Ndiyo, ni kweli mufalme Herode, naye mutawala Pontio Pilato walikusanyika katika muji huu pamoja na Waisraeli na watu wa mataifa mengine kwa kufanya shauri baya juu ya mutumishi wako mutakatifu Yesu, uliyemuchagua kuwa Kristo.


Mutatoa sadaka ya Pasaka kutoka mifugo yenu ya kondoo au ngombe kwa heshima ya Yawe pahali ambapo Yawe atachagua kwa ajili ya jina lake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ