24 Kisha Anasi akamutuma Yesu, akiwa amefungwa, kwa Kayafa Kuhani Mukubwa.
Wale waliomukamata Yesu wakamupeleka kwa Kuhani Mukubwa Kayafa, pahali walimu wa Sheria na wasimamizi wa watu walipokuwa wamekusanyika.
nao Anasi na Kayafa walikuwa Makuhani Wakubwa. Halafu Mungu akatoa ujumbe wake kwa Yoane mwana wa Zakaria katika jangwa.
Wakamupeleka kwanza kwa Anasi. Anasi alikuwa mukwe wa Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mukubwa mwaka ule.
Simoni Petro na mwanafunzi mwingine walimufuata Yesu. Yule mwanafunzi alikuwa akijulikana na Kuhani Mukubwa, kwa hiyo akaingia pamoja na Yesu ndani ya upango wa nyumba ya Kuhani Mukubwa.