Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 18:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Yesu akamujibu: “Nilisema na watu wote waziwazi, nilifundisha siku zote katika nyumba za kuabudia na katika hekalu, pahali Wayuda wote wanapokutana. Sikusema kitu kwa uficho.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 18:20
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Uniokoe toka kinywa cha simba; uokoe nafsi yangu zaifu toka pembe za mbogo hao.


Ninataka kutimiza mapenzi yako, ee Mungu wangu; sheria yako ninaishika kwa moyo wangu wote!”


Mimi sikusema kwa siri, wala katika inchi yenye giza. Mimi sikuwaambia wazao wa Yakobo wanitafute pahali kusipokuwa kitu. Mimi Yawe ninasema ukweli, maneno yangu ni ya kuaminika.


Musogee karibu nami musikie jambo hili: Tangu mwanzo mimi sikusema kwa siri, tangu mambo hayo yaanze kutendeka, nimekuwa pale. Sasa, Bwana wetu Yawe amenituma, na kunipa nguvu ya Roho wake.


“Basi kama watu wakiwaambia: ‘Angalia, Kristo yuko katika jangwa!’, musiende kule. Au wakiwaambia: ‘Angalia, yuko katika chumba cha ndani!’, musiwasadiki.


Kisha Yesu akawaambia watu wale: “Mumekuja na panga na magongo kwa kunikamata kama watu wanavyokwenda kumukamata munyanganyi? Siku zote niliikaa ndani ya hekalu, nikifundisha, nanyi hamukunikamata.


Halafu Kuhani Mukubwa akapasua nguo zake na kusema: “Mutu huyu amemutukana Mungu! Hatuhitaji tena ushuhuda wowote juu yake. Angalia, munatoka kusikia jinsi alivyomutukana Mungu.


Yesu alizunguka katika Galilaya yote akifundisha katika nyumba zao za kuabudia, akihubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha watu waliokuwa na magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.


Yesu alizunguka katika miji na vijiji vyote, akiwafundisha watu katika nyumba zao za kuabudia, akiwahubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.


Yeye aliwaambia maneno hayo waziwazi. Basi Petro akamwita Yesu pembeni na kuanza kumukaripia.


Yesu alikuwa akipitisha muchana katika hekalu akihubiri, na usiku alikuwa akienda kulala kwenye mulima wa Mizeituni.


Alifundisha katika nyumba zao za kuabudia, na kusifiwa na watu wote.


Basi kwa sababu gani unaniuliza mimi? Uwaulize wale waliosikia mambo niliyosema, kwa maana wanajua vizuri nini niliyosema.”


Yesu alisema maneno haya wakati alipokuwa akifundisha katika nyumba ya kuabudia kule Kapernaumu.


Halafu katikati ya sikukuu, Yesu akaingia ndani ya hekalu na kuanza kufundisha.


Angalia, anasema waziwazi wala hawamwambii neno! Labda wakubwa nao wametambua kweli kuwa huyu ndiye Kristo.


Basi Yesu alipokuwa akifundisha katika hekalu akasema hivi kwa sauti: “Ndiyo, ninyi munajidai kwamba munanijua na munajua pahali ninapotoka. Sikukuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini aliyenituma ni mwenye ukweli. Ninyi hamumujui,


Hakuna mutu anayefanya kitu kwa uficho, ikiwa anataka kujulikana waziwazi. Basi kwa kuwa unafanya matendo kama hayo, ujionyeshe mbele ya watu wote.”


Na kesho yake asubui mapema akarudi tena katika hekalu. Watu wote wakamufikia, naye alipoikaa, akaanza kuwafundisha.


Nina maneno mengi ya kusema juu yenu na ya kuwahukumu. Lakini yule aliyenituma ni wa kweli, nami ninajulisha dunia maneno yale niliyosikia kwake.”


Mufalme Agripa anajua vizuri mambo yale yaliyotokea. Nami ninaweza kusema mbele yake pasipo woga kwa maana ninajua hakika kwamba hakuna hata jambo kati ya hayo asilofahamu, kwa sababu hayakufanyika kwa uficho.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ