Yoane 18:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Wakati Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akaondoka pamoja na wanafunzi wake na kuvuka ngambo ya kijito cha Kidroni. Nao wote wakaingia katika bustani iliyokuwa kule.
Daudi alipokuwa akipita pamoja na watu wake, watu wote katika inchi yote walilia kwa sauti. Mufalme Daudi akavuka kijito cha Kidroni pamoja na watu wote, wakapita kuelekea katika jangwa.
Akamwondoa tate yake Maka cheo chake cha mama malkia, kwa sababu alitengeneza sanamu ya Ashera na hiyo sanamu akaivunjavunja na kuiteketeza kwenye bonde la Kidroni.
Mazabahu ambayo wafalme wa Yuda walijenga juu ya paa kwenye chumba cha juu cha Ahazi, pamoja na mazabahu ambayo Manase alijenga katika viwanja viwili vya nyumba ya Yawe, aliyabomoa na kuyapondaponda, kisha alitupa mavumbi yake katika kijito cha Kidroni.
Kisha Yosia akaamuru Kuhani Mukubwa Hilkia na makuhani wasaidizi wake na walinzi wa mulango watoe katika hekalu la Yawe vitu vilivyotengenezwa kwa ajili ya Bali, Ashera na kwa ajili ya jeshi la mbingu. Aliviteketeza inje ya Yerusalema katika bonde la Kidroni na kupeleka majivu yake kule Beteli.
Naye aliondoa sanamu ya Ashera kutoka katika nyumba ya Yawe, inje ya Yerusalema, akaipeleka mpaka kwenye kijito cha Kidroni. Kule akaiteketeza na kuisaga mpaka ikakuwa mavumbi, nayo mavumbi yake akayatawanya juu ya makaburi ya watu.
Mufalme Asa alimwondoa hata mama yake Maka, cheo chake cha malkia, kwa sababu alitengeneza sanamu ya kuchukiza ya Ashera, mungu wa kike. Asa alikatakata sanamu hiyo, akaipondaponda na kuiteketeza kwa moto katika bonde la kijito Kidroni.
Makuhani wakaingia katika sehemu ya ndani ya nyumba ya Yawe, wakatosha uchafu wote uliokuwa mule, wakauweka katika kiwanja. Kutoka pale, Walawi walitwaa uchafu ule mpaka inje kwenye Bonde la Kidroni.
Wakaanza kazi, wakaondoa mazabahu zote zilizokuwa Yerusalema, na zingine zote zilizotumiwa kwa kufukizia ubani, wakazibeba na kuzitupa katika Bonde la Kidroni.
Bonde lote walimozikwa wafu na kutupiwa majivu, mashamba yote, mpaka kijito cha Kidroni, mpaka pembe ya mulango wa Farasi kuelekea upande wa mashariki, litakuwa eneo takatifu kwa Yawe. Hakuna kitakachoharibiwa humo wala kubomolewa tena milele.
Kisha Yesu pamoja na wanafunzi wake wakafika katika bustani inayoitwa Getesemane. Na Yesu akawaambia: “Muikae hapa, kwa wakati ninapokwenda kuomba kule.”
Mutumishi mumoja wa Kuhani Mukubwa, aliyekuwa ndugu ya mutu yule Petro aliyemukata sikio, akamwambia: “Mimi sikukuona kule katika bustani pamoja naye?”
Akatufikia, akatwaa mukaba wa Paulo, akajifunga miguu na mikono yake mwenyewe na kusema: “Roho Mutakatifu anasema: ‘Wayuda watamufunga mutu mwenye mukaba huu namna hii kule Yerusalema na kumutoa kwa watu wa mataifa mengine.’ ”