Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 17:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Nimekujulisha kwao, na nitaendelea kukujulisha kusudi upendo ule unaokuwa nao kwangu ukuwe ndani yao, nami mwenyewe nikuwe ndani yao.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 17:26
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Uniokoe toka kinywa cha simba; uokoe nafsi yangu zaifu toka pembe za mbogo hao.


Na wakati ule mutafahamu kwamba mimi ni ndani ya Baba yangu, na ninyi ni ndani yangu, na mimi ndani yenu.


Yesu akamujibu: “Anayenipenda, atashika maneno yangu. Baba yangu atamupenda, naye Baba pamoja nami tutaingia ndani yake na kukaa ndani yake.


Siwaiti ninyi tena watumishi, kwa sababu mutumishi hajui mambo bwana wake anayofanya. Ninawaita ninyi warafiki kwa sababu nimewajulisha yote niliyosikia kutoka kwa Baba yangu.


Mukae ndani yangu, nami nitakaa ndani yenu. Tawi haliwezi kuzaa matunda lisipokaa ndani ya muzabibu. Vilevile ninyi hamuwezi kuzaa matunda musipokaa ndani yangu.


Kama vile Baba anavyonipenda, mimi ninawapenda ninyi vilevile. Mukae katika upendo huu.


Ninaomba nikuwe ndani yao na wewe ndani yangu, kusudi wapate kuwa mumoja kabisa; na dunia ijue kama wewe ndiwe uliyenituma na kwamba unawapenda kama vile unavyonipenda.


“Nimekujulisha kwa watu wale ulionipa, ukiwachagua katika dunia. Wao walikuwa watu wako, uliwatoa kwangu, nao walishika neno lako.


kwa maana nimewatangazia maneno yale uliyoniagiza, nao wameyakubali. Wamejua hakika kwamba nilitoka kwako na kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anakaa ndani yangu, nami ninakaa ndani yake.


Mimi sijitafutii sifa yangu mwenyewe, lakini kuna mumoja anayeitafuta kwa ajili yangu, naye ndiye mwenye uwezo wa kuhukumu.


Lakini kama Kristo anakaa ndani yenu, ijapokuwa mwili wenu unakufa kwa sababu ya zambi, Roho ndiye uzima wenu kwa maana munahesabiwa haki mbele ya Mungu.


Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.


Kwa maana, Kristo ni kama mwili mumoja unaokuwa na viungo vingi. Ijapokuwa viungo vya mwili ni vingi, vinakuwa mwili mumoja tu.


Na sasa si mimi ninayekuwa ningali nikiishi, lakini ni Kristo anayeishi ndani yangu. Maisha ninayoishi sasa, inatokana na kumwamini Mwana wa Mungu aliyenipenda na kutoa maisha yake kwa ajili yangu.


Basi tumusifu Mungu kwa sababu ya utukufu wa neema yake aliyotujalia kwa njia ya Mwana wake mupendwa.


Hivi Kristo apate kukaa ndani ya mioyo yenu kwa njia ya imani, nanyi mupate kuwa na mizizi na musingi katika upendo.


Ni vigumu sana kuelewa siri hii, lakini ninasema mambo yanayoelekea Kristo na kanisa.


Kwa maana Mungu alitaka kuwafunulia watu hao siri ya mupango wake wenye utajiri mukubwa alioufanya kwa ajili ya mataifa yote. Nayo siri ile ni kwamba Kristo ni ndani yenu, naye ndiye anayetuletea tumaini kwamba tutashiriki katika utukufu wa Mungu.


Na kwa kuungana naye, ninyi mumepata kukamilika. Yeye ndiye anayetawala roho zote zenye mamlaka na uwezo.


Kwa hiyo hakuna tena tofauti kati ya watu wa mataifa mengine na Wayuda, wenye kutahiriwa na wasiotahiriwa, wageni, washenzi, watumwa na watu huru. Lakini Kristo ni yote naye yuko katika wote.


Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatufariji kwa milele na kutupatia tumaini njema,


Kwa maana anasema: “Ee Mungu, nitatangaza jina lako kwa wandugu zangu, nitakusifu katikati ya mukutano.”


Mutu anayetii amri za Mungu anakaa ndani yake, na Mungu anakaa ndani ya yule mutu. Tunatambua kwamba Mungu anakaa ndani yetu kwa njia ya Roho Mutakatifu aliyetupatia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ