Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 17:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Uwatakase wapate kujitoa kwako kabisa kwa njia ya ukweli, maana yake kwa njia ya neno lako la kweli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 17:17
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa, ee Bwana wangu Yawe, wewe ndiwe Mungu, na maneno yako ni kweli. Umeniahidi mimi mutumishi wako jambo hili jema.


Kwa kanuni zako ninapata hekima, kwa hiyo ninachukia kila mwenendo mubaya.


Nimeshika neno lako ndani ya moyo wangu, kusudi nisikukosee.


Maagizo yako ni ya haki siku zote; unijalie akili nipate kuishi.


Kifungo cha neno lako ni ukweli, maamuzi yako yote ya haki yanadumu milele.


Namna gani kijana ataweza kujichunga katika njia safi? Ni kwa kufuatilia neno lako.


Lakini Yawe anasema: “Kwa sababu wamasikini wanaugua, na wakosefu wanalia, sasa ninasimama, nami nitawapa usalama wanaoutazamia.”


“Basi hii ndiyo maana ya ule mufano wa mupandaji: mbegu ni mufano wa neno la Mungu.


Nao udongo muzuri walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mwema na kwa uhaki. Ndio wale wanaovumulia hata wanatoa matunda mazuri.


Ninyi mumekwisha kuwa safi kwa kuwa mumeshika maneno niliyowaambia.


Ninajitoa kwako kabisa mimi mwenyewe kwa ajili yao, kusudi wao vilevile wapate kujitoa kwako kabisa.


Halafu mutajua ukweli, na ukweli utawaweka huru.”


Lakini sasa munatafuta kuniua ijapokuwa nimewaambia ukweli niliousikia kutoka kwa Mungu. Abrahamu hakufanya vile.


Yeye hakufanya ubaguzi kati yetu na wao; ametakasa mioyo yao kwa sababu walimwamini.


Sisi wote ambao uso haukufunikwa, tunaonyesha kama kioo utukufu wa Bwana. Kwa hiyo, tunabadilishwa kwa kufanana na Bwana, nasi tunapita toka utukufu mumoja hata utukufu mwingine unaokuwa mukubwa zaidi tena. Kwa maana kazi hii inatimizwa na Bwana ndiye Roho.


Hakika mumesikia habari zake, nanyi mukiwa waamini mumefundishwa kufuatana na ukweli unaokuwa ndani ya Kristo.


Alifanya hivi kusudi atakase kanisa kwa ajili ya Mungu, akilisafisha kwa maji na kwa neno.


Lakini sisi tunapaswa kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wandugu wapendwa wa Bwana. Kwa maana Mungu amewachagua ninyi wa kwanza kuwa watu wake kusudi mupate kuokolewa kwa kutakaswa na Roho Mutakatifu na kwa kuamini maneno ya ukweli.


Kwa sababu hiyo, mutupilie mbali mambo yote machafu na matendo ya uovu yanayozidi. Mupokee kwa unyenyekevu neno lile lililopandwa ndani yenu na linaloweza kuwaokoa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ