Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 16:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Kutakuwa wakati, nao umetimia, ndio wakati mutakaposambazwa, kila mutu akijiendea ngambo yake mwenyewe, nanyi mutaniacha peke yangu. Lakini mimi si peke yangu kabisa, kwa sababu Baba yuko pamoja nami.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 16:32
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Usiku huu ninyi wote mutaanguka kwa ajili yangu, kwa maana imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: ‘Nitamwua muchungaji, na kondoo wa kundi watasambazwa.’


Mambo haya yote yamefanyika kusudi maneno yanayosemwa na manabii katika Maandiko Matakatifu yapate kutimia.” Basi wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.


Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ninyi wote mutaanguka, kwa maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Nitamwua muchungaji, na kondoo watasambazwa.’


Wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.


Yesu akawajibu: “Saa ya kutukuzwa kwa Mwana wa Mutu imetimia.


Watawatenga musiingie katika nyumba za kuabudia. Na kutakuwa wakati ambapo wote watakaowaua watazani kwamba wanamutumikia Mungu.


“Nimewaambia ninyi maneno hayo kwa mifano. Lakini kutakuwa wakati sitasema nanyi tena kwa mifano, lakini nitawaambia ninyi waziwazi juu ya Baba.


Na kisha akamwambia yule mwanafunzi: “Sasa huyu ndiye mama yako.” Na tokea saa ile, mwanafunzi yule alimupeleka Maria kwake.


Kisha mambo hayo hawa wanafunzi wawili wakarudi kwao.


Yesu akamwambia: “Ee mama, unisadiki; kutakuwa wakati hamutamwabudu Baba juu ya mulima huu wala Yerusalema.


Lakini kutakuwa wakati, nao umekwisha kutimia, wale wanaoabudu kwa kweli watakapomwabudu Baba katika roho na ukweli; kwa maana Baba anataka watu wanaoabudu kwa namna ile.


Kweli, kweli ninawaambia: kutakuwa wakati, nao umekwisha kutimia, wafu watakaposikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale wanaoisikia, wataishi.


Musishangae kwa ajili ya maneno haya, kwa sababu kutakuwa wakati wafu wote wanaokuwa ndani ya makaburi watakaposikia sauti yake


Lakini hata ningehukumu, hukumu yangu ingekuwa ya kweli, kwa sababu sihukumu peke yangu, lakini Baba aliyenituma ni pamoja nami.


Yule aliyenituma ni pamoja nami; hakuniacha peke yangu, kwa sababu siku zote ninafanya maneno yanayomupendeza.”


Kisha kuagana, tukaingia ndani ya chombo, nao wakarudi kwao.


Naye Saulo alikuwa amekubali kwamba Stefano anastahili kuuawa. Siku ile ile kanisa lililokuwa katika Yerusalema lilianza kupata mateso makubwa. Waamini wote walisambaa katika Yudea na Samaria, isipokuwa mitume tu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ