Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 16:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 “Siku ile itakapotimia, ninyi hamutaniuliza juu ya kitu fulani. Kweli, kweli ninawaambia: Baba atawapa chochote mutakachomwomba kwa jina langu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 16:23
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata mbele hawajaniita, mimi nitawaitikia; mbele hawajamaliza kusema, nitakuwa nimewajibu.


Na kitu chochote mutakachoomba, mukiamini, mutakipata.”


“Muombe, nanyi mutapewa; mutafute, nanyi mutapata; mupige hodi, nanyi mutafunguliwa mulango.


Na wakati ule mutafahamu kwamba mimi ni ndani ya Baba yangu, na ninyi ni ndani yangu, na mimi ndani yenu.


Yuda (si yule Yuda Iskariota) akamwuliza: “Bwana, namna gani utajitambulisha mwenyewe kwetu wala si kwa dunia?”


Toma akamwambia: “Bwana, hatujui pahali unapokwenda, basi namna gani tutajua njia?”


Kama mukikaa ndani yangu na maneno yangu yanakaa ndani yenu, mutaomba chochote munachotaka, nanyi mutakipewa.


Yesu alitambua kwamba walitaka kumwuliza. Basi akawaambia: “Munaulizana juu ya maneno niliyosema kwamba kunabaki wakati kidogo nanyi hamutaniona, lakini kisha wakati kidogo mutaniona tena?


Siku ile itakapotimia, mutamwomba Baba kwa jina langu. Mimi sisemi kwamba nitawaombea ninyi kwa Baba,


Sasa tunajua kwamba unajua yote na si lazima mutu akuulize kitu. Sababu hii tunaamini kama ulitoka kwa Mungu.”


Kwa maana, kwa njia ya Kristo sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, tumefunguliwa njia ya kufika mbele ya Baba katika Roho mumoja.


Watoto wangu wapendwa, ninawaandikia maneno hayo kusudi musitende zambi. Lakini kama mutu akitenda zambi, tuko na yule anayetutetea mbele ya Baba. Naye muteteaji yule ndiye Yesu Kristo, mwenye haki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ