Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 16:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Wakati mwanamuke anapozaa, anasikia uchungu kwa sababu wakati wake wa kuzaa umetimia. Lakini anapokwisha kuzaa, hakumbuki tena maumivu, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa kwa mutoto.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 16:21
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha akamwambia mwanamuke: “Nitakuzidishia uchungu wa kuzaa, Utazaa watoto kwa uchungu. Utakuwa na hamu na mume wako, naye atakutawala.”


Utazisahau taabu zako zote; utazikumbuka tu kama mafuriko yaliyopita.


Anamurudishia heshima mwanamuke anayekuwa tasa; anamufurahisha kwa kumujalia watoto. Haleluia!


Watu watafazaika, watashikwa na hofu na maumivu, watakuwa na uchungu kama mama anapozaa. Wataangalia kwa mashaka, nyuso zao zitaungua kwa haya.


Kwa maono hayo nimeingiwa na woga mukubwa. Maumivu mengi yamenishika, kama maumivu ya mama anayezaa. Nimefazaika zaidi hata siwezi kusikia; nimefazaika hata siwezi kuona.


Muji wangu mutakatifu, ni kama mama anayezaa bila kupata uchungu; mbele ya uchungu kuanza, amekwisha zaa mutoto.


Enyi watu wa Sayuni, mulie na kugaagaa kama mwanamuke anayezaa! Maana sasa mutaondoka katika muji huu muende kukaa katika mbuga, mutakwenda mpaka Babeli. Lakini kule, mutaokolewa. Kule Yawe atawakomboa toka katika makucha ya waadui zenu.


Sasa kwa nini munalia kwa sauti? Hamuna mufalme tena? Mushauri wenu ametoweka? Munalalamika kwa uchungu, kama mwanamuke anayezaa!


Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Ufurahi wewe tasa, ushangilie, upige kelele wewe usiyejua uchungu wa kuzaa. Kwa maana muke aliyeachwa na mume, atakuwa na watoto wengi kuliko yule anayekuwa naye.”


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ