Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 16:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 “Kunabaki wakati kidogo, ninyi hamutaniona; lakini kisha wakati kidogo mutaniona tena.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 16:16
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Bwana Yesu alipokwisha kusema nao maneno hayo, akanyanyuliwa juu kwenda mbinguni na kuikaa kwa upande wa kuume wa Mungu.


Yesu akawaambia: “Mwangaza ungali kati yenu kwa muda kidogo. Mutembee wakati mungali na mwangaza, kusudi giza lisiwafunike, kwa sababu anayetembea katika giza hajui pahali anapokwenda.


Yesu alijua kwamba Baba yake ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, na kwamba yeye mwenyewe alitoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.


Watoto wangu, ningali pamoja nanyi kwa muda mufupi tu. Mutanitafuta, lakini sawasawa nilivyowaambia Wayuda, ninawaambia ninyi vilevile kwamba hamuwezi kufika pahali ninapokwenda.


Kuelekea haki ni kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamutaniona tena.


Na sasa ninyi vilevile munasikia uchungu, lakini nitawaona tena, nanyi mutafurahi, wala hakuna mutu atakayeweza kuwahuzunisha tena.


Nilitoka kwa Baba, nami nimekuja katika dunia. Sasa ninaacha dunia na kurudi kwa Baba.”


Sasa ninarudi kwake yule aliyenituma na hakuna mumoja wenu anayeniuliza kwamba ninaenda wapi.


Lakini sasa ninarudi kwako, nami ninasema maneno haya nikingali katika dunia, kusudi furaha yangu kubwa kabisa ikuwe ndani yao.


Na sasa, Baba, unipe utukufu karibu nawe, utukufu unaokuwa sawa na ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuumbwa kwa dunia.


Yesu akasema: “Ningali pamoja nanyi kwa wakati kidogo na kisha nitarudi kwa yule aliyenituma.


Nyuma ya kufa kwake, alijionyesha kwao kwa namna nyingi kwa kuhakikisha kwamba amefufuka. Kwa muda wa siku makumi ine, alionekana kwao na kusema nao juu ya maneno yanayoelekea Ufalme wa Mungu.


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ