Yesu akawaambia: “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mungenipenda, kwa maana nimetoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikukuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini yeye ndiye aliyenituma.
Siku moja alipokuwa akikusanyika pamoja nao, akawaagiza: “Musitoke Yerusalema, lakini mubaki kule mukingojea zawadi ambayo Baba yangu aliahidi, ile niliyowaambia ninyi.
Naye Mungu anayejua mafikiri ya mutu, alihakikisha kwamba amewakubali watu wa mataifa mengine kwa njia ya kuwapatia Roho Mutakatifu sawa vile alivyotupatia sisi.
Mungu vilevile alihakikisha ushuhuda wao kwa njia ya maajabu, ya miujiza mbalimbali, na ya vitambulisho, na kwa njia ya zawadi za Roho Mutakatifu alizowapa watu kama anavyopenda.
Kisha yule malaika akanionyesha muto wa maji ya uzima wenye kungaa kama kioo, uliokuwa ukitiririka toka kwenye kiti cha kifalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo.