Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 15:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Siwaiti ninyi tena watumishi, kwa sababu mutumishi hajui mambo bwana wake anayofanya. Ninawaita ninyi warafiki kwa sababu nimewajulisha yote niliyosikia kutoka kwa Baba yangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 15:15
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe ni rafiki ya wale wanaomwabudu; yeye anawajulisha agano lake.


Warafiki wengi wanaweza kumwangusha mutu, lakini kuna rafiki mwaminifu kuliko ndugu.


Hakika, Bwana wetu Yawe hafanyi kitu bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake.


Akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa mbinguni, lakini kwao si vile.


Kisha Yesu akawageukia wanafunzi wake wakiwa peke yao, akawaambia: “Heri watu wanaoona mambo yale munayoona!


Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.


Kweli, kweli ninawaambia: mutumishi si mukubwa kuliko bwana wake, wala mujumbe si mukubwa kuliko yule aliyemutuma.


Mukumbuke maneno niliyowaambia kwamba mutumishi si mukubwa kuliko bwana wake. Kama walinitesa mimi, watawatesa ninyi vilevile. Na kama walishika maneno yangu, watashika maneno yenu vilevile.


“Ningali na maneno mengi ya kuwaambia, lakini sasa hamujakuwa na uwezo wa kuyafahamu.


Nimekujulisha kwao, na nitaendelea kukujulisha kusudi upendo ule unaokuwa nao kwangu ukuwe ndani yao, nami mwenyewe nikuwe ndani yao.”


Yesu akamwambia: “Usinishike, kwa sababu sijapanda bado kwa Baba. Lakini kwenda kwa wandugu zangu na kuwaambia kwamba ninapanda kwa Baba yangu anayekuwa Baba yenu vilevile, anayekuwa Mungu wangu na Mungu wenu vilevile.”


Halafu mwanamuke yule akamwambia: “Bwana, ninaona kama wewe ni nabii.


Nina maneno mengi ya kusema juu yenu na ya kuwahukumu. Lakini yule aliyenituma ni wa kweli, nami ninajulisha dunia maneno yale niliyosikia kwake.”


Ni vile kwa sababu niliwatangazia mupango wote wa Mungu pasipo kuwaficha kitu.


Hakika sijui kitu ninachofanya. Kwa maana kile ninachotaka kufanya, sikifanyi; lakini kile ninachochukia, ndicho ninachofanya.


Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Ni nani anayejua mawazo ya Bwana? Ni nani anayeweza kumushauria?” Lakini sisi tuko na mawazo yanayotoka kwa Kristo.


Mungu alituma Roho wa Mwana wake ndani ya moyo wetu kwa kuhakikisha ya kuwa ninyi ni wana wake. Roho anayetuombea, akiita: “Baba!”


Ametujulisha mipango yake iliyokuwa imefichwa; ndiyo ile aliyokusudia kwa mapenzi yake tangu mbele kwamba ataitimiza kwa njia ya Kristo.


Zamani, Mungu hakuwajulisha watu mupango ule sawa vile ameujulisha sasa kwa mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho wake.


Neno lile ndio ile siri aliyoificha tangu zamani za kale, lakini sasa ameifunua kwa watu wake.


Kwa sababu sasa yeye si kama vile mutumwa tu, lakini amekuwa bora zaidi kuliko mutumwa: yeye ni ndugu mupendwa. Mimi ninamupenda sana, nawe utamupenda zaidi sana, kwanza kama vile mutumwa, tena kama vile ndugu katika Bwana.


Barua hii inatoka kwangu mimi Yakobo, mutumishi wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo. Ninawasalimia ninyi watu wa makabila kumi na mawili waliosambazwa katika dunia.


Na maandiko haya yakatimia: “Abrahamu alimwamini Mungu na kwa hiyo akahesabiwa kuwa mwenye haki.” Na Mungu akamwita rafiki yake.


Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao alitangulia kushuhudia mateso yatakayomupata Kristo na utukufu utakaokuwa nyuma. Nao walijitolea kusudi wapate kuvumbua wakati gani na kwa njia gani mambo haya yatafanyika.


Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.


Barua hii inatoka kwangu mimi Yuda, mutumishi wa Yesu Kristo na ndugu wa Yakobo. Ninawaandikia ninyi mulioitwa na Mungu Baba na munaoishi katika upendo wake na kulindwa kwa ajili ya Yesu Kristo.


Hizi ni habari za mambo yaliyofunuliwa na Yesu Kristo. Kristo alipata ufunuo huu kutoka kwa Mungu, kusudi awaonyeshe watumishi wake mambo yanayopaswa kutokea kisha kidogo. Kristo alimutuma malaika wake kwa kumujulisha mutumishi wake Yoane mambo yale.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ