Si wewe, ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa inchi hii wakati watu wako Waisraeli walipoingia katika inchi hii, ukawapa wazao wa Abrahamu rafiki yako, ikuwe yao milele?
Nao walifika, wakaitwaa na kuirizi. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na hasara hii.
Basi, nikafanya kama nilivyoamriwa. Siku hiyo, wakati wa muchana, nikafunga muzigo wangu kama muzigo wa mutu anayekimbia. Magaribi nikatoboa ukuta na giza lilipokuwa likiingia, nikatoka, nikibeba muzigo wangu juu ya mabega, watu wote wakiniona.
“Anayekubali amri zangu na kuzitii, ni yeye anayenipenda. Baba yangu atamupenda yule anayenipenda, na mimi nitamupenda vilevile na nitajitambulisha kwake.”
Mumesikia jinsi nilivyowaambia kwamba ninajiendea, lakini nitawarudilia tena. Kama mungenipenda, mungefurahia kujua kwamba ninakwenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mukubwa kuliko mimi.