13 Hakuna anayekuwa na upendo mukubwa kuliko mutu anayetoa maisha yake kwa ajili ya warafiki zake.
“Ninawaambia ninyi warafiki zangu: musiwaogope wale wanaoua mwili tu lakini hawawezi kufanya kitu kingine zaidi.
“Mimi ni muchungaji mwema. Muchungaji mwema anatoa maisha yake kwa ajili ya kondoo wake.
kama vile Baba anavyonijua mimi, na mimi ninavyomujua Baba. Vilevile mimi ninatoa maisha yangu kwa ajili ya kondoo wangu.
Ninajitoa kwako kabisa mimi mwenyewe kwa ajili yao, kusudi wao vilevile wapate kujitoa kwako kabisa.
Muishi katika upendo kama vile Kristo alivyotupenda na kutoa maisha yake kwa ajili yetu kama vile matoleo na sadaka ya kuteketezwa kwa moto yenye harufu nzuri inayomupendeza Mungu.
Sisi tumetambua upendo kwa njia hii: Yesu Kristo alitoa uzima wake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kutoa uzima wetu kwa ajili ya wandugu zetu.