4 Munajua njia ya kufika pahali ninapokwenda.”
Haikumupasa Kristo ateswe kama vile na aingie kwenye nafasi atakapotukuzwa?”
Mimi ni mulango. Mutu akiingia kwa kupitia kwangu, ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata chakula.
Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.
Yesu alijua kwamba Baba yake ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, na kwamba yeye mwenyewe alitoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.
Ndani ya nyumba ya Baba yangu kuna nafasi nyingi za kukaa. Isingekuwa hivi singewaambia kwamba ninakwenda kuwatayarishia nafasi.
Mumesikia jinsi nilivyowaambia kwamba ninajiendea, lakini nitawarudilia tena. Kama mungenipenda, mungefurahia kujua kwamba ninakwenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mukubwa kuliko mimi.
Nami nitakapokwisha kuwatayarishia ninyi nafasi, nitarudi tena na kuja kuwatwaa, kusudi pahali nitakapokuwa, ninyi mupate kuwa pale vilevile.
Toma akamwambia: “Bwana, hatujui pahali unapokwenda, basi namna gani tutajua njia?”
Nilitoka kwa Baba, nami nimekuja katika dunia. Sasa ninaacha dunia na kurudi kwa Baba.”
Anayemwamini Mwana yuko na uzima wa milele. Anayekataa kumwamini Mwana hatapata uzima; atakaa akipatwa na kasirani ya Mungu.”
Hakika mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mutu anayemwona Mwana na kumwamini apate uzima wa milele, nami nitamufufua siku ya mwisho.”