Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoane 14:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Nami nitakapokwisha kuwatayarishia ninyi nafasi, nitarudi tena na kuja kuwatwaa, kusudi pahali nitakapokuwa, ninyi mupate kuwa pale vilevile.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoane 14:3
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.


Mumesikia jinsi nilivyowaambia kwamba ninajiendea, lakini nitawarudilia tena. Kama mungenipenda, mungefurahia kujua kwamba ninakwenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mukubwa kuliko mimi.


Munajua njia ya kufika pahali ninapokwenda.”


“Baba, ninataka wale ulionipa wakuwe pamoja nami pahali nitakapokuwa, nao waone utukufu wangu, ndio ule utukufu ulionipa kwa sababu ulinipenda mbele ya kuumbwa kwa dunia.


Watu hao wakawaambia: “Ninyi Wagalilaya, sababu gani munasimama pale mukiangalia mbinguni? Huyu Yesu aliyenyanyuliwa toka katikati yenu kwenda mbinguni, atarudi sawa vile mulivyomwona akienda.”


Na kama sisi ni watoto, basi tutakuwa na sehemu katika urizi ule Mungu aliowaahidi watu wake, na tutashiriki pamoja na Kristo katika urizi ule; kwa maana kama tukiteswa pamoja naye tutatukuzwa pamoja naye vilevile.


Maana ninasongwa na mambo mawili. Ninatamani kujiendea na kukaa pamoja na Kristo, maana hili ndilo jambo bora zaidi.


Kwa hivi mutatukuza jina la Bwana wetu Yesu, nanyi mutatukuzwa naye kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.


Kama tunaendelea kuvumilia, tutatawala pamoja naye vilevile. Kama tunamukana, naye atatukana vilevile.


Hivi vilevile Kristo naye alijitoa kufa mara moja kusudi aondoe zambi za watu wengi. Naye atarudi tena, si kwa ajili ya kuondoa zambi, lakini kwa kuwaokoa wale wanaomungojea.


Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ