25 “Nimewaambia maneno haya kwa maana ningali sasa pamoja nanyi.
Ninawaambia ninyi sasa hayo yote mbele hayajatokea, kusudi wakati yatakapotokea, mwamini kwamba ‘Mimi Ndimi.’
Asiyenipenda hashiki maneno yangu. Na neno munalosikia nikisema halitoki kwangu, lakini linatoka kwa Baba yangu aliyenituma.
Lakini Musaidizi, ndiye Roho Mutakatifu, yule Baba atakayemutuma kwa jina langu, atawafundisha maneno yote na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Nimewaambia maneno haya sasa mbele hayajatokea, kusudi wakati yatakapotokea, mupate kuamini.
“Nimewaambia ninyi maneno haya kusudi mufurahi sawa mimi, na furaha yenu ikuwe kubwa kabisa.
“Ningali na maneno mengi ya kuwaambia, lakini sasa hamujakuwa na uwezo wa kuyafahamu.