Lakini kama nikiyatenda, hata ikiwa hamuniamini mimi, basi mwamini matendo yangu, kusudi mupate kujua kabisa kwamba mimi na Baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu, nami ndani yake.”
Hauamini kwamba mimi na baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu na mimi ndani yake? Maneno ninayowaambia siyasemi kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini Baba anayekaa ndani yangu ndiye anayefanya kazi zake.
Mimi sitabaki tena katika dunia, lakini wao wangali katika dunia na mimi ninakuja kwako. Baba Mutakatifu, uwalinde kwa uwezo wa jina lako, lile jina ulilonipa, kusudi wakuwe mumoja kama vile sisi tunavyokuwa mumoja.
Munisalimie wanainchi wenzangu Androniko na Yunia, waliofungwa pamoja nami katika kifungo. Wao wanasifiwa sana kati ya mitume, nao walikuwa katika Kristo mbele yangu.
Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.
Ninamujua mutu mumoja aliyeungana na Kristo, na sasa kumekwisha kupita miaka kumi na mine, mutu huyu akanyanyuliwa mpaka katika mbingu ya tatu. (Ikiwa alinyanyuliwa katika hali ya kimwili au ya kiroho mimi sijui, Mungu peke yake anajua.)
Mujichunguze ninyi wenyewe kusudi mupate kujua kama munasimama imara katika imani. Mujipime. Si munajua kwamba Yesu Kristo anakaa kati yenu? Kama si vile ni kusema kwamba mumeshindwa.
Ndiyo kusema, Mungu ndiye aliyekuwa akipatanisha watu wote na yeye mwenyewe kwa njia ya Kristo bila kuhesabu makosa yao. Yeye ametupatia ujumbe wa upatanisho.
Na sasa si mimi ninayekuwa ningali nikiishi, lakini ni Kristo anayeishi ndani yangu. Maisha ninayoishi sasa, inatokana na kumwamini Mwana wa Mungu aliyenipenda na kutoa maisha yake kwa ajili yangu.
Kwa maana sisi ni viumbe vya Mungu, na kwa kuungana kwetu na Yesu Kristo, alituumba kusudi tuishi maisha ya matendo mema, ambayo Mungu alitutayarishia tangu mbele tupate kuyatenda.
Kwa maana Mungu alitaka kuwafunulia watu hao siri ya mupango wake wenye utajiri mukubwa alioufanya kwa ajili ya mataifa yote. Nayo siri ile ni kwamba Kristo ni ndani yenu, naye ndiye anayetuletea tumaini kwamba tutashiriki katika utukufu wa Mungu.